Na John Gagarini, Lugoba
Wagombea
wa nafasi za uongozi hapa nchini wametakiwa kukubali matokeo mara
uchaguzi utakapofanyika Oktoba 25 mwaka huu kwani kuna maisha mengine
baada ya uchaguzi, na kuendelea kufanya kampeni zao huku wakiendelea
kuhubiri na kulinda amani iliyopo kwani wana nafasi kubwa ya
kuwashawishi wafuasi wao wasifanye vurugu au kufanya vitendo
vinavyosababisha uvunjifu wa amani.
Pia
wagombea watakaoshindwa kwenye uchaguzi mkuu wameombwa wakubali matokeo
kwani kwenye washindani lazima kuwe na washindwa ili kuondoa hali ya
mafarakano kwani kwa wale watakaoshindwa wasipokubali matokeo wanaweza
kuleta uvunjifu wa amani.
Hayo
yalisemwa katika Kijiji cha Maviayangombe kata ya Lugoba wilayani
Bagamoyo mkoani
Pwani na Askofu mkuu wa Dayosisi ya Morogoro ya Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania (KKKT) Jacob Mameo Ole Paulo wa Dayosisi ya Morogoro
wakati wa mazishi ya mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa wafugaji Laban
Moreto, Karokya Moreto (33) ambaye alikuwa mwanajeshi wa kikosi cha
04/691 cha Mtwara.
Askofu
Ole Paulo alisema kuwa wagombea hao wanauwezo wa kudumisha amani kwa
kuhubiri au kuingiza nchi kwenye machafuko endapo watayatumia vibaya
majukwaa wakati wa kipindi hichi cha kampeni za uchaguzi. watoto watatu.
Baadhi ya akinamama ambao ni ndugu wakaribu wakilia
Jeneza lenye mwili wa marehemu likiwa limebebwa na wanajeshi ukiwasili makaburini
Baadhi ya Wazee wakiwa wamekaa kwenye msiba huo huko kijiji cha Maviyangombe Lugoba wilayani Bagamoyo.
Kulia
ni Ridhiwani Kikwete mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM
akifuatiwa na mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga, mkuu wa wilaya ya
Nachingwea Pololet Mgema na mgombea ubunge Jimbo hilo kupitia Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Matayo Torongei wakiwa kwenye msiba
huo.






No comments:
Post a Comment