Mapema akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kimadawa Kenya (KEMRI), Musau Kyanesa amesema
lengo la kuanzishwa kwa PAMCA ni kutafuta njia stahiki ya kupambambana na mdudu
mbu ambae hueneza magonjwa mbalimbali ambayo huathiri binadamu.
“Itakuwa ni jambo jema sana kama tutaweza kumdhibiti mdudu huyu mbu ambaye anaeneza
magonjwa haya na kufanikiwa kwa hilo tutaweza kuendeleza afya za wananchi wetu
kwa nchi za Afrika, maana Afrika ndio tunapata shida sana na mdudu huyu mbu,”
alisema Kyanesa.
Aidha
Kyanesa ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa KEMRI amesema wameandaa mpango
wa kuhamasisha wanafunzi vyuoni kujikita katika sayansi ya Mbu ili
kupata watalaam wengi wakuweza kukabiliana mbu Kenya na Afrika kwa
ujumla.
“Tunaandaa
mpango wa kuhamasisha vijana kusomea na hatimaye kuwa na utaalm juu ya
mapambano na kufanya tafiti za mbu, kwa kugharamia masomo yao kutokana
na upungufu wa wataalam kulingana na tatizo lenyewe,”alisema Kyanesa.
|
No comments:
Post a Comment