KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

November 27, 2015

WAZIRI MKUU WA JIMBO INDIA APIGA MARUFUKU MATUMIZI YA POMBE

Waziri mkuu wa jimbo la Bihar nchini India ,Nitish Kumar (pichani) ametangaza mipango ya kupiga marufuku uuzaji na utumizi wa pombe katika jimbo hilo.
Bwana Kumar awali alikuwa amewaahidi wapiga kura kwamba atazuia ufunguaji wa maduka ya kuuza pombe katika vijiji.
Hatua hiyo italigharimu jimbo la Bihar zaidi ya dola milioni 500 za kodi,kulingana na msemaji wa chama tawala cha Bihar Janata Dal.
Pombe imepigwa marufuku katika majimbo kadhaa ya India ikiwemo Gujarat na Manipur.
Bwana Kumar anaongoza muungano wa vyama vya kijimbo vilivyochukua mamlaka katika jimbo la Bihar mapema mwezi huu.
Wakati wa kampeni zake,alikabiliwa na maandamano ya wanawake ambao walilalama kuhusu ubugiaji mbaya wa pombe katika vijiji.

No comments:

Post a Comment