![]() |
Msemaji wa chama cha Forum for
Democratic Change Ssemujju Ibrahim Nganda amethibitisha kwamba mgombea
urais wa chama hicho Dkt Kizza Besigye aliyekuwa amekamatwa na polisi
sasa ameachiliwa huru.
Kanali huyo mstaafu ambaye ni kigogo wa
upinzani nchini Uganda alikuwa amekamatwa katika kitongoji cha Naguru,
mjini Kampala katika nyumba ambayo upinzani ulidai wizi wa kura ulikuwa
ukifanyika.Wafuasi wa upinzani, wakiambatana na kanali Besigye, wanadai walifumania watu wakiiba kura na wakataka usaidizi wa polisi kukagua nyumba hiyo lakini wakazuiliwa. Besigye alikamatwa na maafisa wa polisi walioondoka naye kutoka eneo hilo. Haijabainika alipelekwa wapi. |
February 19, 2016
BESIGYE AACHIWA NA POLISI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment