KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 19, 2016

BESIGYE AACHIWA NA POLISI

Msemaji wa chama cha Forum for Democratic Change Ssemujju Ibrahim Nganda amethibitisha kwamba mgombea urais wa chama hicho Dkt Kizza Besigye aliyekuwa amekamatwa na polisi sasa ameachiliwa huru.
Kanali huyo mstaafu ambaye ni kigogo wa upinzani nchini Uganda alikuwa amekamatwa katika kitongoji cha Naguru, mjini Kampala katika nyumba ambayo upinzani ulidai wizi wa kura ulikuwa ukifanyika.
Wafuasi wa upinzani, wakiambatana na kanali Besigye, wanadai walifumania watu wakiiba kura na wakataka usaidizi wa polisi kukagua nyumba hiyo lakini wakazuiliwa.
Besigye alikamatwa na maafisa wa polisi walioondoka naye kutoka eneo hilo.
Haijabainika alipelekwa wapi.

No comments:

Post a Comment