Aliyekuwa katibu mkuu wa FIFA Jerome Valcke amepigwa marufuku kushiriki katika soka yoyote kwa kipindi cha miaka 12.
Uamuzi
huo umeafikiwa na kamati ya maadili ya shirikisho hilo kufuatia madai
ya uovu yanayohusishwa na uuzaji wa tiketi za michuano ya kombe la
dunia.Wakati wa uchunguzi ,visa kadhaa vya uovu vilijitokeza ,ikiwemo matumizi ya nauli,sera na taratibu. Valcke pia amepigwa faini ya faranga 100,000 za Uswizi ambazo ni sawa na pauni 70,800. |
No comments:
Post a Comment