KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 20, 2016

MKURUGENZI WA VODACOM TANZANIA,IAN FERRAO ATINGA CLOUDS FM NA EFM RADIO LEO

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao(kulia) pamoja na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakimsikiliza Mkuu wa Vipindi wa  Clouds  FM,Sebastian Maganga(watatu kulia)  alipokuwa akiwafafanulia  jambo  juu ya studio ya kurushia vipindi vinavyofanywa na kituo hicho, wakati wa ziara maalum iliyofanywa na Uongozi wa kampuni hiyo  kwa ajili ya mafunzo mbalimbali na kuendeleza mahusiano mazuri ya kibiashara na kituo hicho kilichopo   jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga (kushoto) na Mkurugenzi wa Vipindi wa kituo hicho, Ruge Mtahaba (kulia)  wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa  Vodacom Tanzania, Ian Ferrao,( katikati ) alipokuwa akifafanua jambo juu ya utendaji mzuri wa kituo Clouds TV na Clouds FM, wakati alipouongoza  Uongozi wa kampuni hiyo  kutembelea  makao makuu ya kituo hicho jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali na kuendeleza mahusiano mazuri ya kibiashara.

Mkurugenzi Mtendaji wa  Vodacom Tanzania, Ian Ferrao,(kulia )  akimsikiliza Mkurugenzi wa Vipindi   wa  Clouds Media Group, Ruge Mtahaba(kushoto) alipokuwa akimuelezea jinsi shughuli mbalimbali za utangazaji zinavyoendeshwa na kituo hicho,wakati wa ziara maalumu iliyoongozwa na Mkurugenzi huyo kutembelea kituo hicho  jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali na kuendeleza mahusiano mazuri ya kibiashara.

Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga  akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa  Vodacom Tanzania, Ian Ferrao( kushoto )  alipotembelea makao makuu ya kituo hicho  jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali na kuendeleza mahusiano mazuri ya kibiashara na kituo hicho,katikati Materi Mushi.

No comments:

Post a Comment