Mwenyekiti
wa CCM, Rais Kikwete akionyesha jengo lililokuwa Ofisi ya TANU mkoa wa
Singida miaka ya 75 akiwa katibu msaidizi wa TANU wa wilaya
Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akipiga picha na mke wake Mama Salma Kikwete, leo, mbele ya nyumba ambamoishi mjii Singida mwaka 1975, wakati huo akiwa katibu Msaidizi wa TANU wilaya
ya Singida mjini. Kikwete yupo mkoani Singida kwa ajili ya kuongoza
Maadhimisho ya Miaka 39 ya CCM, abayo kilele chake kitaifa ni kesho
JK akisalimiana na wazee alipowasili kuzungumza nao mjini Singida leo
…………………………………………………………………………………………………..
Na Richard Mwaikenda,Singida
MWENYEKITI CCM, Rais mstaafu
Jakaya Kikwete, amewaomba wazee kote nchini, kumuunga mkono Rais John
Magufuli katika uongozi wake ili kumpa
moyo wa kuwatumikia Watanzania. Alisema,
kipindi ambacho Dk Magufuli ameingia madarakani hadi sasa ni mda mfupi,
hivyo si vema kuanza kudodosa na kulaumu panapopwaya, badala yake Wazee
na watanzania kwa jumla wazidi kumuunga mkono ili kumtia moyo wa
kutekeleza yote aliyokusudia kuyafanya kwa manufaa ya taifa.
Kikwete alitoa ombi hilo
alipokuwa akizungumza katika mkutano na wazee wa Mkoa wa Singida, ambapo
alisema kuwa kuongoza bila ushauri wa wazee nchi inaweza kuyumba.
“Kuongoza nchi bila wazee
mambo hayaendi vizuri na ukikosa mzee kwenye jahazi wapiga makasia
vijana wanaweza kuanza kuzozana na chombo kwenda mrama, lakini wakiwepo
wazee watawaongoza vizuri na chombo/ nchi kwenda salama”. Alisema
Kikwete huku akishangilia na wazee.
Si Kila mzee ni mwasisi wa chama, kila mwenye mvi na mwasisi, wengine wameingia kwenye chama wazee.
Alisisitiza kwamba ukitaka nchi
itulie kamata wazee, lakini ukiongoza nchi kwa kutumia vijana pekee
nchi inaweza kuyumba, na itafika mahali mtakosa mahali pa kushika.
Alisema kuwa hata yeye kwa mara ya kwanza .alipokwenda kuomba ubunge
jimboni kwake Bagamoyo, Pwani aliunda kamati ya wazee ambayo ilimsaidia
sana.
Wazee ni sehemu ya matumaini ya
chama na Serikali, panapokuwepo wazee hapaharibiki jambo. “Nawashukuru
sana wazee endeleeni kukijenga chama na kuiunga mkono Serikali
inayoongozwa sasa na Dk John Magufuli.” Alisisitiza Kikwete na kuongeza
kuwa,
“Hata kwenye chama chetu
tumeunda Baraza la Washauri la Wazee wasitaafu, ambapo wengi walipinga,
hata hao wazee tuliowataka waunde baadhi yao walipinga, lakini mwisho
walikubali kwa masharti kwamba wawe wanaitwa panapotokea jambo kubwa
litakalohitaji ushauri wao.”
Alisema mmoja wa viongozi
aliyekuwa msitari wa mbele kuunda baraza hilo, alikuwa Rais msitaafu wa
Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ambaye alitoa ushauri wa kuitwa kutoa
ushauri panapotokea jambo kubwa na kwamba hata wakitoa ushauri, viongozi
waliopo madarakani wawe hiari kuukubali au kuukataa’.
Aliwataka wazee kuendelea
kuiunga mkono serikali ya sasa ambayo kwa hivi sasa imetimiza muda mfupi
wa miezi mitatu ambaye ni sawa na mtoto mdogo anayekua.
Alisema kuwa Jambo kubwa ni
kuwaunga mkono, kuliko kuwalaumu ama sivyo watavunjika moyo, ndani ya
miaka mitano itakuwa hasara. watieni moyo ili wajiamini wahudumie vizuri
zaidi ili nchi isonge mbele kimaendeleo.
Kikwete alisisitiza kuwa hata
yeye akitakiwa kwenda kutoa ushauri atakwenda, na akiwa na jambo la
kushauri atakwenda pia, lakini aliwaasa kuwa si kila jambo wazee watake
kwenda kutoa ushauri, itachelewesha mambo mengi.
JK akisalimiana na wazee alipowasili kwenye mkutano ambapo alizungumza na wazee wa mkoa wa Singida
JK akiwasili katika mkutano na wazee wa Mkoa wa Sindida leo
Katibu
wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungmza kabla ya kumkaribisha Mke
wa Mwenyekiti wa CCM, Salma Kikwete kuzungumza na wazee wa Mkoa wa
Singida
Mama Salama Kikwete akizungumza katika mkutano huo
Katibu wa Baraza la Wazee Mkoa wa Singida,Athuman Sima akisoma risala mbele ya Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete
Mwenyekiti
wa Baraza la Wazee Mkoa wa Singida, Juma Mudida akiapa mbele ya Jakaya
Kikwete kuwa yupo tayari kupambana na mtu yeyote alatayepingana na
utumbuaji wa majipu unaofanywa na Rais Magufuli
Jakaya
Kikwete akizungumza katika mkutano na wazee amabapo amewaomba kuunga
mkono uongozi wa Rais John Magufuli ili nchi isonge mbele kimaendeleo.
Baadhi ya wazee wakiondoka baada ya kuzungumza na JK mjini Singida leo
|
No comments:
Post a Comment