KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 5, 2016

SAKATA LA MATESO YA WANAFUNZI WA TZ INDIA, POLISI WATATU WASIMAMISHWA KAZI

Polisi watatu wamesimamishwa kazi kwa muda mjini Bangalore nchini India kwa tuhuma za kukataa kusikiliza na kupokea malalamiko ya watu walioshambuliwa na kundi la watu ambapo mwanafunzi mmoja wa kike kutoka Tanzania alivuliwa baadhi ya nguo zake. 

Polisi wamesema pia wamekamata watu wanne zaidi kuhusiana na shambulio hilo, na kufikisha idadi ya waliokamatwa kufikia tisa. 

Kundi la watu lilimshambulia na kumvua nguo mwanamke mwenye umri wa miaka 21, baada ya gari la mwanafuzi kutoka Sudan kumgonga na kumuua mwanamke mmoja wa Kihindi. 

Tukio hilo limetokea eneo la Hessarghatta siku ya jumapili. Eneo hilo lina vyuo kadhaa ambapo kuna idadi kubwa ya wanafunzi kutoka Afrika, wakiwemo 150 kutoka Tanzania.

No comments:

Post a Comment