KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 12, 2016

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI ATEMBELEA WILAYA ZA WANGING’OMBE NA MAKAMBAKO

ms1      Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe, Assumpter Mshama akizungumza mbele ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Wanging’ombe (WINGISA), Philemon Luhanjo.
ms2
  Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge akiwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Mwenyekiti wa Bodi ya WINGISA, Philemon Luhanjo, Meneja WINGISA, Inj. Najib Asumbwile (mwisho kulia) na Mkurugenzi Msaidizi wa Maji Vijijini, Inj. Jackson Mutazamba (mwisho kushoto) pamoja na wafanyakazi wa WINGISA.
ms3
  Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge akitembelea chanzo cha maji cha Fukulwa, Wilaya ya Makambako.
ms4
   Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge akiwa na Mbunge wa Jimbo la Makambako, Deo Sanga na Mkuu wa Wilaya ya Makambako, Sarah Dumba wakiwa kwenye eneo la ujenzi la Bwawa la Tagamenda, Wilaya ya Makambako.
ms5
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge akizungumza na wananchi wa Manga, Wilaya ya Makambako.
………………………………………………………………………………………………………………….
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge leo ametembelea Wilaya za Wanging’ombe na Makambako mkoani Njombe na kujionea hali ya utekelezaji wa miradi ya maji kulingana na ahadi ya Mhe. Rais, John Magufuli katika kampeni zake za urais. Aidha, ziara yake hiyo imelenga kuhakikisha kuwa miradi inayosuasua inatekelezwa na kuisha kwa wakati ili kutatua kero ya maji kwa wananchi kulingana na Sera ya Maji ya Mwaka 2002, kutimiza lengo la ifikapo mwaka 2025 wananchi wote mijini na vijijini wawe wanapata maji kwa asilimia mia.
Vilevile, Inj. Lwenge alifika kwenye Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Wanging’ombe (WINGISA) kujionea utendaji wa mamlaka hiyo na kuzungumza na wafanyakazi wake kwa nia ya kuboresha utendaji wake.

No comments:

Post a Comment