Mrimbwende
Zawadi Dotto (Pichani) ameibuka kidedea katika Mashindano ya Miss
Albinism Kanda ya Ziwa yaliyofanyika usiku wa Kuamkia leo Jijini Mwanza.
Miss
Zawadi mwenye umri wa miaka 17 (mwanafunzi) ameibuka mshiki katika
Mashindano hayo ambayo ni maalumu kwa ajili ya Watu wenye ulemavu wa
ngozi kwa ajili kuonyesha umahiri wao katika tasnia ya urimbwene hii
ikiwa pia ni ishara ya kwamba watu wenye ulemavu wa ngozi wanaweza
kushiriki katika shughuli na mashindano mbalimbali.
Mashindano
hayo yanaandaliwa na Taasisi ya kusaidia Watu wanaoishi katika
Mazingira hatarishi iitwayo SAVE VUNERABLE FOUNDATION ya Jijini Dar es
Salaam.
Mratibu
wa Shirika hilo Alexander Exaud Mutowo ametanabaisha kwamba, baada ya
mashindano hayo kukamilika kwa kanda zote nchini, Washindi wa Kanda hizo
watashindanishwa Jijini Dar es salaam ili kumpata Mshindi wa Kitaifa wa
MISS ALBINISM 2016.
Wshiriki
Saba wa Miss Albinism 2016 Kanda ya Ziwa na umri wao katika mabano
ambapo kutoka Kushoto ni Hajra Sadru (22), Antonia Mathias William (17),
Furaha Edward John (17), Pendo Faustine (15), Zabibu Abdallah (18),
Zawadi Dotto (17) pamoja na Asteria Christopher.
Washiriki walioingia Nne bora ambapo kutoka kushoto Hajra Sadru, Furaha Edward, Zabibu Abdallah na Zawadi Dotto
Baada
ya Mtifuano mkali hatimae majaji wakatangaza washini. Furaha Edward
mshindi wa tatu (Kushoto), Hajru Sadru mshindi wa pili (katikati) na
Zawadi Dotto akaibuka kuwa mshindi wa Kwanza (aliepiga magoti).
Mshindi
wa Miss Albinism Kanda ya Ziwa akivikwa taji lake. Wa pili kulia ni
Jalia Mtani ambae alikuwa Jaji Mkuu akitajana Majina ya washindi.
Pembeni ni Mshereheshaji Emmanuel Shalali kutoka Sahara Media Group.
No comments:
Post a Comment