Kocha Mkuu wa Mbeya City Fc, Kinnah Phiri ametangaza majina ya
nyota 18 watakaoivaa Simba Sports Club kwenye mchezo wa ligi kuu ya
Vodacom Tanzania bara uliopangwa kuchezwa jumapili hii kwenye uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam
Mapema leo Phiri ameuambia mtandao huu kuwa anatua jijini Dar na
kikosi cha nyota hao ambao aliwaandaa maalumu kwa mchezo huo wa mwishoni
mwa juma akiwa na imani kubwa kuwa wataiwezesha City kuibuka na ushindi
kutokana na ‘kuiva’ vizuri kimazoezi na mafunzo waliyoyapata katika
wiki nzima ya maandalizi kupitia mifumo mbalimbali aliyokuwa
akiifundisha .
“Nina imani nao,wamefanya vizuri sana kwenye mazoezi ya
wiki hii, sina shaka na wao kutupatia matokeo kwa sababu wako sawa
tayari kwa mchezo,tutacheza kwenye mfumo mpya ambao haujawahi kuonekana
tukicheza, hii ni kwa sababu tumedhamiria kupata ushindi kama ambavyo
timu imekuwa ikifanya kila inapokutana na Simba”, alisema.
Miongoni mwa nyota walio kwenye orodha ya kuivaa Simba siku hiyo ya
jumapili ni pamoja na mlinzi Hassan Mwasapili, mlinda lango Haningtony
Kalyesubula pia wamo Temi Felix, Haruna Shamte,Yohana Moriss,Kenny
Ally,Geoffrey Mlawa,Issa Nelson na wakali wengine 10 ambao wamepewa
majukumu kadhaa kuhakikisha City inaandikisha pointi tatu muhimu mbele
ya timu hiyo ya Msimbazi.
Huu utakuwa ni mchezo wa sita kwa timu hizi kukutana katika michuano
hii ya ligi kuu ya vodacom huku City ikifanikiwa kushinda mara mara
mbili sare mbili na Simba ikishinda mara moja katika michezo mitano
iliyozikatanisha timu hizi hapo awali.
No comments:
Post a Comment