KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 4, 2016

WAZIRI PROF. MBARAWA AKAGUA BARABARA YA TABORA-KOGA-MPANDA KM 356

2
Muonekano wa Daraja la Koga baada ya kufanyiwa ukarabati kufuatia kuathiriwa na mvua kubwa zilizonyesha katika mkoa wa Katavi. Daraja hilo kwa sasa linaruhusu magari kupita ya tani 1 hadi 3.
3
Muonekano wa barabara ya Tabora-Koga-Mpanda yenye urefu wa Km 356 inayojengwa kwa kiwango cha lami ikiwa katika hatua za awali za ujenzi wake.
4
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa mkandarasi wa kampuni ya CICO anayejenga barabara ya Tabora-Koga- Mpanda yenye urefu wa Km 356, sehemu ya Tabora-Sikonge kumaliza mradi huo kwa wakati.
5
Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Bi. Hanifa Sirengu akitoa taarifa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu hali ya miundombinu katika wilaya yake.
6
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) wakati alipotembelea kiwanja cha ndege cha Tabora.
7
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisikiliza maelezo ya namna vifaa vya kuongozea ndege vinavyofanya kazi kutoka kwa mtaalamu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), mkoa wa Tabora.

No comments:

Post a Comment