KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 29, 2016

REAL MADRID MABINGWA WAPYA WA UEFA CHAMPION LEAGUE, WAITANDIKA ATLETICO MADRID PENATI 5-4

ZINWachezaji wa timu ya Real Madrid wakishangilia mara baada ya kuwafunga wapizani wao Atletico Madrid katika mchezo wa fainali ya klabu bingwa ya Ulaya UEFA Champions League uliofanyika kwenye uwanja wa San Siro  Milan, Italy uliomalizika usiku huu.
ima
Dk 15, Ramos anaiandikia Madrid bao la kwanza kwa kuunganisha mpira wa kupara wa kichwa wa Bale
  Ni dakika ya 12, Madrid wamefanikiwa kufanya angalau mashambulizi matatu lakini bado hakuna bao.
Inaonekana Madrid wana kasi zaidi wanapoingia upande wa Atletico.
Kila upande umeanza mechi kwa kasi na kunaonekana kuna presha kubwa.
Sasa ni Mapumziko timu zote zimeingia vyumbani kwa ajili ya mapumziko ngoja tuone Kocha Zinedine wa Real Madrid na Kocha Diego Simeone wa Atletico Madrid wataleta mabadiliko gani katika kipindi cha pili kinachotarajiwa kuanza mara baada ya dakika 15 za mapumziko
zine
Kocha Zinedine Zidane wa Real Madrid akihamasisha wachezaji wake kucheza kwa kujituma katika mchezo wa fainali dhidi ya mahasimu wao  timu ya Atletico Madrid katika mchezo wao unaofanyika nchini Italia hivi sasa Atletico Madrid wanakosa penati ambayo imepigwa na mchezaji Antoine Griezmann baada ya mchezaji wa timu Real Madrid  Fernado Torres kuanguswa katika eneo la hatari.
Lakini kwa sasa huenda Real Madrid wakaongeza tena mashabulizi ili angalau kutoka na ushindi katika mchezo huo na kuchukua uchampioni wa ligi ya klabu bingwa ulaya,  Hata hivyo si kazi rahisi ngoja tuone mwelekea wa mchezo unavyoenda katika dakika 90 za mchezo huo.Lakini kwa sasa huenda Real Madrid wakaongeza tena mashabulizi ili angalau kutoka na ushindi katika mchezo huo na kuchukua uchampioni wa ligi ya klabu bingwa ulaya,  Hata hivyo si kazi rahisi ngoja tuone mwelekea wa mchezo unavyoenda katika dakika 90 za mchezo huo.
carvasoMchezaji wa Atletico Madrid Yannick Ferreira Carrasco akishangilia mara baada ya kufunga goli la kusawazisha katika dakika ya 89 ya mchezi kipindi cha pili.
Mchezaji wa Carrasco wa Atletico Madrid anaisawazishia goli timu yake katika dakika ya 89 ya mchezo  na matokeo kuwa Real Madrid 1-Atletico madrid -1,  mpira umekwisha na  zinaongezwa dakika  30 , baada ya hapo kama hatapatikana mshindi timu zitaingia katika uamuzi wa kupiga penati tano kila timu ili kupata mshindi katika mchezo huo
PENATI ZINAPIGWA SASA
 Sasa dakika 30 za nyongeza zimekwisha timu zinaingia tena uwanjani kwa ajili ya kupiga penati 5 kila moja ukumbuke kwamba upigaji wa penati unategemea sana uwezo wa magolikipa kuzuia penati langoni lakini poia upigaji mzuri wa penati kwa wachezaji wa uwanjani  hebu tungoje na tuone ni timu gani inao uwezo katika penati lakini pia ni golikipa gani ana uwezo mzuri wa kuzuia penati  katika ya Keylor Navas wa Real Madrid na Jan Oblak wa Atletico Madrid.
Christiano Ronaldo anapiga penati ya tano na ya ushindi na kuitangazia dunia kuwa klabu ya Real Madrid inachukua ubingwa wa klabu bingwa za vilabu ulaya kwa kuwafunga wapinzani wao wakubwa nchini Hispania Real Atletico kwa penati 5-4 mara baada ya mchezaji wa timu ya Atletico Madrid  Juanfran kukosa penati ya nne katika mchezo huo hivyo Real Madrid wanachukua ubingwa wa Klabu Bingwa Ulaya UEFA Champions League Hongereni Real Madrid Hongera Kocha Zinedine Zidane

No comments:

Post a Comment