Wachezaji
wa timu ya Real Madrid wakishangilia mara baada ya kuwafunga wapizani
wao Atletico Madrid katika mchezo wa fainali ya klabu bingwa ya Ulaya
UEFA Champions League uliofanyika kwenye uwanja wa San Siro Milan,
Italy uliomalizika usiku huu.
Kocha Zinedine Zidane wa Real
Madrid akihamasisha wachezaji wake kucheza kwa kujituma katika mchezo wa
fainali dhidi ya mahasimu wao timu ya Atletico Madrid katika mchezo
wao unaofanyika nchini Italia hivi sasa Atletico Madrid wanakosa penati
ambayo imepigwa na mchezaji Antoine Griezmann baada ya mchezaji wa timu Real Madrid Fernado Torres kuanguswa katika eneo la hatari.
Lakini kwa sasa huenda Real
Madrid wakaongeza tena mashabulizi ili angalau kutoka na ushindi katika
mchezo huo na kuchukua uchampioni wa ligi ya klabu bingwa ulaya, Hata
hivyo si kazi rahisi ngoja tuone mwelekea wa mchezo unavyoenda katika
dakika 90 za mchezo huo.Lakini kwa sasa huenda Real
Madrid wakaongeza tena mashabulizi ili angalau kutoka na ushindi katika
mchezo huo na kuchukua uchampioni wa ligi ya klabu bingwa ulaya, Hata
hivyo si kazi rahisi ngoja tuone mwelekea wa mchezo unavyoenda katika
dakika 90 za mchezo huo.
Mchezaji
wa Atletico Madrid Yannick Ferreira Carrasco akishangilia mara baada ya
kufunga goli la kusawazisha katika dakika ya 89 ya mchezi kipindi cha
pili.
Mchezaji wa Carrasco wa Atletico
Madrid anaisawazishia goli timu yake katika dakika ya 89 ya mchezo na
matokeo kuwa Real Madrid 1-Atletico madrid -1, mpira umekwisha na
zinaongezwa dakika 30 , baada ya hapo kama hatapatikana mshindi timu
zitaingia katika uamuzi wa kupiga penati tano kila timu ili kupata
mshindi katika mchezo huo
PENATI ZINAPIGWA SASA
Sasa dakika 30 za nyongeza
zimekwisha timu zinaingia tena uwanjani kwa ajili ya kupiga penati 5
kila moja ukumbuke kwamba upigaji wa penati unategemea sana uwezo wa
magolikipa kuzuia penati langoni lakini poia upigaji mzuri wa penati kwa
wachezaji wa uwanjani hebu tungoje na tuone ni timu gani inao uwezo
katika penati lakini pia ni golikipa gani ana uwezo mzuri wa kuzuia
penati katika ya Keylor Navas wa Real Madrid na Jan Oblak wa Atletico
Madrid.
Christiano Ronaldo anapiga penati
ya tano na ya ushindi na kuitangazia dunia kuwa klabu ya Real Madrid
inachukua ubingwa wa klabu bingwa za vilabu ulaya kwa kuwafunga
wapinzani wao wakubwa nchini Hispania Real Atletico kwa penati 5-4 mara
baada ya mchezaji wa timu ya Atletico Madrid Juanfran kukosa penati ya
nne katika mchezo huo hivyo Real Madrid wanachukua ubingwa wa Klabu
Bingwa Ulaya UEFA Champions League Hongereni Real Madrid Hongera Kocha
Zinedine Zidane
No comments:
Post a Comment