Kocha wa Leicester Claudio Ranieri
anataka 'staili ya sinema' ambayo itawaiwezesha timu yake maarufu kama 'mbweha' kunyakua ubingwa ugenini uwanja wa Old Trafford baadaye leo.
Ushindi huo wa ugenini utaiwezesha Leicester City kunyakua ubingwa ugenini huku wakiwa wamewaacha wanaowafuatia kileleni Tottenham kwa pointi saba na bado Leicester wakiwa na michezo miwili kibindoni.
Hata kama hawatashinda leo , bado wanahitaji pointi tatu katika mechi tatu walizobakiza kutawazwa mabingwa
"Huwezi amini, hii ni historia, na tunafahamu ," anasema Ranieri raia wa Italia.
"Ni vizuri kumalizia stori kama sinema . Fainali huwa ni safi na mwisho mzuri.
Ranieri alijiunga na Leicester Juni mwaka jana |
Msimu uliopita Leicester ilinusurika kushuka daraja, sasa hivi imeandika historia kwa mafanikio waliyoyapata.
sawa
ReplyDelete