KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 13, 2016

WAFANYABIASHARA BARANI AFRIKA WATAKIWA KUUNGANISHA NGUVU KUPAZA SAUTI ZAO

arusha
Umoja wa wafanyabiashara barani Afrika umewataka wafanyabiasha barani humu kuungana na kupaaza sauti zao ilikuweka mazingira bora ya kufanyabiashara zao kwenye nchi za bara hili.
Wakizungumza kwenye mkutano wao wa siku mmoja uliofanyika jijini hapa wamesema mazingira ya ufanyajibiashara kwenye nchi za bara hili umekuwa na utofauti hali inayowawia vigumu kutoa biashara sehemu moja kwenda nyingine.
Akizungumza kwenye mkutano huo mwenyekiti wa umoja huo Peter otafire ambaye pia ni waziri wa afya wa Uganda amesema kuwa mazingira hayo yamekuwa yakisababisha ukuaji wa rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.
Alisema kuwa kumekuwa na muingiliano wa asili kwenye nchi zetu katika mipaka kwa watu kufanyabiashara toka zama mpaka walipotugawa wakoloni nasi hadi sasa viongozi wa serikali zetu hawajaweka mazingira bora yaliokuwepo toka zama hizo.
Alisema kuwa kumekuwepo na wajasiriamali wadogo ambao mpaka Leo wameshindwa kunyanyuka kibiashara sababu ya urasimu usio walazima na kuzitaka serikali za bara hili kuheshimu ripoti ya utafiti wa raisi mstaafu Thabo Mbeki.
”Nadhani imefika wakati kwetu kubadilika kama tunataka maendeleo ya kiuchumi kwa watu wetu na kuwepo mazingira bora ya uganyaji biashara kwa sisi wenyewe kwenye bara hili”alisisitiza brigedia jenerali Otafire.
Nae mfanyabiashara kutoka nchini Kenya Mahmoud Othao alisema kuwa kitu Kidogo au rushwa imekuwa chachu ya kutofikiwa malengo kwa wafanyabiasha kwenye mataifa YETU barani hapa hali inayowafanya kushindwa kufikiwa kwa malengo tarajiwa.
Alisema kuwa sehemu kubwa ya wafanyabiashara wamekuwa wabinafsi kuwasaidia wenzao wajasiriamali kuinuka hali inayositisha ukuaji wa kiuchumi na kutosaidiana huko kunapelekea kutokuwepo na mazingira mazuri ya mipango endelevu na urasimu kwa watunga Sera kuegamia wachache.
Mkutano huo uliokuwa ukijadili ujasiriamali na mikakati ya kuukuza ilikuweza kuleta matokeo chanya kwa wajasiriamali barani Afrika utakaopelekea kuleta maendeleo ya kiuchumi

No comments:

Post a Comment