Siku
mbili baada ya kuhukumiwa kifungo cha miezi 18 gerezani kwa kosa la
kumpiga teke dansa wake wa kike, Koffi Olomide ameachiwa huru na kurejea
uraiani.
Taarifa
ya Koffi kuachiwa huru imetolewa na promota wa Kenya aliyemwalika
katika onyesho lililofanyika mwisho mwa wiki iliyopita, Jules Nsana
ambaye alisema kuwa aliwasiliana na Koffi na kumweleza kuwa yupo
nyumbani na familia yake.
“Nilizungumza
na Olomide akiwa nyumbani kwake na akaniambia kuwa ameruhusiwa. Aikuwa
na bendi yake, marafiki na familia . Ninafuraha na hilo,” alisema Nsana.
Koffi
alitiwa katika mikono ya dola Julai, 26 akiwa nyumbani kwake na
kuhumiwa kifungo cha miezi 18 gerezani kwa kosa la kumpiga mmoja wa
madansa wake wa kike baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Jommo
Kenyata nchini Kenya ambako alikuwa amekwenda kwa ajili ya kutumuiza
katika onyesho.
|
July 29, 2016
HUKUMU YA MIEZI 18 KWA KOFFI OLOMIDE YAYEYUKA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment