KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 24, 2016

OPARESHENI UKUTA: MSAJILI WA VYAMA AITISHA MAZUNGUMZO YA SIKU MBILI KWA VYAMA VYOTE ILI KUSAKA SULUHU

SeeBait
MSAJILI wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, ameitisha Baraza la Vyama vya Siasa ili kunusuru mvutano uliojitokeza kati ya Jeshi la Polisi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Jaji Mtungi amevitaka vyama vya siasa vilivyotangaza kufanya maandamano na mikutano isiyo na tija nchi nzima kuacha, badala yake warudi kwenye meza ya mazungumzo ili kuondoa tofauti zinazojitokeza.

Kauli ya Jaji Mutungi imekuja baada ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) nao kutangaza maandamano ya amani kwa ajili ya kupongeza utendaji kazi wa Rais Dk. John Magufuli, huku Chadema kikiitisha maandamano na mikutano isiyo na kikomo nchi nzima, ambayo imepewa jina la Operesheni Ukuta.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Jaji Mutungi alisema kufanyika kwa maandamano na mikutano hiyo, hakuwezi kuondoa changamoto za kisiasa zilizopo, hivyo basi wanapaswa kukaa kwenye meza moja kwa ajili ya kujadili tofauti zilizopo na kuzipatia ufumbuzi.

“Ninawaomba wale wote wenye lengo la kuitisha maandamano na mikutano ya kisiasa kuacha kwa sababu haiwezi kusaidia kuondoa changamoto zilizopo, bali tunapaswa kukaa kwenye meza moja ya mazungumzo ili tuweze kujadili tofauti hizo na kuzipatia majibu,” alisema Jaji Mutungi.

Aliongeza kuwa licha ya kuwapo kwa jitihada za viongozi mbalimbali kujadili suala hilo, lakini vyama hivyo vimeonekana bado vikiendelea na misimamo yao ya kuitisha mikutano na maandamano yasiyo na kikomo, jambo ambao linaweza kuleta hofu kwa wananchi.

Jaji Mutungi alisema katika kipindi hiki ambacho wananchi wametulia, hakuna haja ya kuwatia hofu au wasiwasi ili ionekane kuwa nchi ina ombwe kubwa la uongozi, jambo ambalo linaweza kurudisha nyuma juhudi za kuleta maendeleo.

No comments:

Post a Comment