Chuo
cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kinatarajia kufanya kongamano maalum
la maadhimisho ya kumbukizi ya Mwalimu Nyerere 14 Oktoba,2016 huku Mada
Kuu ikiwa ni: Miiko ya Uongozi na Azimio la Arusha.
Akizungumza
na waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam mapema leo 12 Oktoba,2016
Mkuuu wa Chuo hicho, Profesa. Shadrack Mwakalila ameinisha kuwa
kongamano hilo ni maalum katika kumuenzi Mwalimu Nyerere tokea kifo
chake kilichotokea miaka 17 iliyopita.
“Lengo
ni kumuenzi kwa viendo. Hivyo watu mbalimbali wageni waalikwa na watoa
mada wataelezea namna ya Miiko ya uongozi na namna Azimio la Arusha.
Mada
juu ya Azimio la Arusha itatolewa na Dkt. Harun Kondo huku Mada ya
Miiko ya Uongozi itatolewa na Mh.Wilson Mkama, Mh. Joseph Butiku. Pia
wapo Mh. Ibrahimu Kaduma na Mh. Phillip Mangula” amesema Mkuu wa chuo
huyo, Profsa Mwakalila.
Aidha,
amesema kuwa, tukio hilo litafanyika chuoni hapo katika ukumbi wa
Utamaduni ambapo viongozi mbalimbali wa Kiserikali, binafsi na wananchi
wengine wanaalikwa na ni bure ilikuweza kujifunza namna ya falsa za Baba
wa Taifa katika misingi imara ya maadili ya kazi na utawala


No comments:
Post a Comment