KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 12, 2016

MTOTO MIEZI NANE ATELEKEZWA NA MAMA YAKE WETE PEMBA

indexMTOTO wa kike anayekisiwa kuwa na umri kati ya miezi minane na mwaka mmoja amefikishwa katika Ofisi ya Ustawi wa Jamii Wilaya ya Wete na wasamaria wema  baada ya kutekelezwa na mama yake mzazi.
 
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika Ofisi ya Ustawi wa Jamii Wilaya ya Wete , Amina Ali Mabrouk mkaazi wa Bopwe Jimbo la Gando  ambaye aliachiwa mtoto huyo na mama yake  , alisema mama mzazi wa mtoto huyo alimtelekeza mwanawe siku ya Jumatatu  jioni kwa madai anakwenda kutelekeza ibada ya sala ya jioni .
 
Alieleza kwamba baada ya kukabidhiwa kichanga hicho , mama mzazi hakutokea tena ambapo alichukua hatua za kwenda kuripoti  kituo cha polisi Wete kwa hatua za kisheria kwa kuwa mtoto huyo alikuwa anahitaji huduma  .
 
“Nilikuwa katika biashara zangu kigengeni , mara alitoa mama mmoja hanijui wala na mimi simjui , alinitaka nimsaidie mtoto ili aende kutekeleza ibada ya sala lakini kuanzia muda huo sikumuona tena ”alieleza.
 
Aidha aliongeza kwamba “Ilipofika saa nne usiku ilinibidi niende kutoa taarifa kwa sheha na baadaye Polisi ambapo nilitakiwa nimfike leo (jana) asubuhi ,  nimefika mapema nikaambiwa nije ofisi ya Ustawi wa jamii ”aliongeza.
 
Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya hiyo Salma Suleiman amekiri kupokea kichanga hicho na kusema hatua ya kwanza ni kumpeleka hospitali kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake huku hatua nyingine zikiendelea kuchukuliwa .
 
Alisema katika kuhakikisha mama mzazi anapatikana , Ofisi ya ustawi wa jamii imeanza kuwasiliana na viongozi wa shehia ili kusaidia kupatikana mama yake ambapo kwa sasa ataendelea kuhifadhiwa na Ofisi ya Ustawi wa jamii.
 
“Jambo la kwanza ambalo Ofisi ya Ustawi itafanya ni kumpeleka Hospitali kufanyiwa uchunguzi w afya mtoto huyo , halafu masuala mengine ya kumtafuta mama mzazi zitafuatia baadaye ”alieleza.

No comments:

Post a Comment