KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 27, 2016

DK. SHEIN: SMZ KUENDELEA KUTOA ELIMU NA AFYA BURE

indexAli Issa na Mwanaisha Mohamed Maelezo Zanzibar
Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Baloz Seif Ali Iddi kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi dkt Ali Mohamed Shein  amesema Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kutoa elimu bila malipo na Afya kwa wananchi wake hapa visiwani.
Hayo ameyasema leo huko chuo cha Afya Mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar wakati alipokuwa katika Mahafali  ya Pili na ya 23  ya Chuo cha Taaluma ya Sayansi ya madaktari.
Amesema Serikali inatambua umuhimu wa elimu na Afya kwani ndio njia mojawapo ya kuleta maendeleo,hivyo haina budi kuitoa huduma hiyo bila malipo kwanindio njia maojapo  yakuleta  maendeleo katika nchi .
Aidha alifahamisha kua chuo cha Sayansi ya taaluma ya Afya kwa sasa hakitakua tena chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya bali kitakua kipochini ya uangalizi wa SUZA.
Alisema kupelekwa huko ni kupata frusa nyingi pamoja na soko la ajira kutanuka.
Dkt. Shein alisema kuwa muajiriwa yoyote katika utumishi wa umma atalazimika kufanya kazi popote ndani ya nchihii kama alivyo tia saini makataba na hatasubutu kukataa sehemu alio pangiwa kufanyakazi.
Nae Waziri wa Afya Mahamuod Thabiti Kombo  aliwataka wahitimu hao kufanya kazi kwa uadilifu wakizingatia lugha wanazo zitoa ziwe lugha tabibu ili mgonjwa aridhike na matibabu na kupona haraka.
Alisema madaktari na wauguzi watumie uzalendo wanapo wahudumia wagonjwa na kuthamini kazizao wao wakiwa ni watu muhimu katika nchi.
Jumla ya wahitimu 525walitunukiwa vyeti  Chuoni hapo kwa kiwango cha stashahada ya uguzi,Afya na Mazingira,Afisa Tabibu,Afya ya kinywa na Meno,Utabibu na Maabara na madawa

No comments:

Post a Comment