KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 27, 2016

JESHI LA POLISI KASKAZINI PEMBA LATOA ELIMU KWA WATOTO

poli1
Makame Ali Makame Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polsi akisisitiza jambo kuhusu matumizi mabaya ya simu za mikononi kwenye mkutano wa kuelimisha wanafunzi wa skuli ya sekondari Kizimbani iliyoko  mjini Wete kupinga matendo ya udhalilishaji pamoja na njia bora ya kuwaheshimu walimu baada ya kuibuka tabia ya kurushiwa chupa za mikojo walimu wawapo darasani na baadhi ya wanafunzi wanaojiita manunda
poli2
Mmoja wa Viongozi wa dini akizungumza na wanafunzi wa skuli ya Kizimbani sekondari wilaya ya Wete juu ya kuibuka vitendo vya kurushiwa chupa za mikojo walimu na wanafunzi wanapokuwa darasani .
poli3
Afisa kutoka Dawati la Jinsia na Watoto kutoka  jeshi la polisi mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Juma Salum akitoa elimu ya kupinga matendo ya udhalilishaji kwa wanafunzi wa skuli ya sekondari Kizimbani wilaya ya Wete.
………………………………………………………………………..
Na  Masanja Mabula –Pemba ..
JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba kupitia kitengo cha Dawati la Jinsia na watoto limeanza kutekeleza mpango mkakati wa  kukabiliana na matendo ya udhalilishaji wa kijinsia ikiwemo  wa ulawiti na utumiaji wa madawa za kulevya .
Katika utekelezaji wa mkakati huo , watendaji wa jeshi la Polisi kitengo cha Dawati la jinsia na watoto wameanza ziara ya kuzitembelea skuli za mjini Wete na kuzungumza na wanafunzi , walimu pamoja na wazazi wa wanafunzi walioacha masomo kutokana na sababu mbali mbali .
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mkuu wa dawati la Jinsia Jeshi la Polisi Mkoani hapa Khamis Faki Simai alisema kwamba ziara hiyo pia zinatumika kuwarejesha skuli wanafunzi walioacha masomo pamoja na wanaokaa nje ya madarasa wakati wa  masomo .
Amesema uwamuzi wa kutekeleza mpango mkakati huo ni kutaka kupunguza matendo ya udhalilishaji wa kijinsia ikiwemo yale ya ulawiti na utumiaji wa dawa za kulevya yanayowaathiri zaidi vijana waliochini ya umri wa miaka 18.
Alifahamisha kwamba katika utekelezaji wa mpango mkakati huo , wameweza kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa walimu na wazazi wa wanafunzi ambao wameahidi kutoa ushirikiano wao ambao wamekuwa wakiambana katika zoezi la utoaji wa elimu kwa jamii .
“Mpango mkakati ambao tumeanza kuutekeleza umelenga kutokomeza vitrndo vya udhalilishaji wa kijinsia ikiwemo ya ulawiti pamoja na utumiaji wa dawa za kulevya kwani tumelenga kuhakikisha kunakuweko na jamii yenye maadili ”alifahamisha.
Naye Salama Juma kutoka kitengo cha dawati la Jinsia alisema jeshi la Polisi linatambua umuhimu wa elimu katika kukuza uchumi wa nchi , hivyo wameamua kuwarejesha wanafunzi skuli ili wakapate haki yao ya msingi .
Alisema katika ziara na mikutano ambayo wameifanya imesaidia kuwarejesha baadhi ya wanafunzi skuli waliokuwa wameacha skuli pamoja na kuwafanya kuhudhuria masomo wanafunzi watoro .ambapo pia ameahidi kufanya ufuatiliaji wao .
Mmoja wa wazazi Ali Omar Kanchape amabaye mtoto wake alikuwa ni miongoni wa waliokuwa wameacha skuli , alilishukuru jeshi la Polisi kuendesha mpango mkakati huo ambao umesaidia kijana wake kurejea skuli .
Aliwataka wazazi na walezi kuupokea kwa mtizamo chanya mpango huo na kuhakikisha wanashiriki katika kuwaelimisha wanafunzi walioacha skuli pamoja na watoto wa kupindukia kutambua faida ya elimu na hasara ya kuikosa kwake .
Kassim Thinei mwanafunzi wa kidato cha pili Skuli ya Mitiulaya  ambaye alikuwa ametoroka skuli ya kipindi kirefu aliwataka vijana wenzake ambao wameacha skuli kurejea na kuendelea na masomo na kuachana na makundi maovu ambayo hatma yake ni kujiingiza kwenye vitendo viovu .
Jeshi la Polisi limeanza kutekeleza mpango mkakati huo , huku kukiwa na taarifa mbaya za ongezeko la vijana wanajihusha na matendo ya ulawiti katika Wilaya ya Wete

No comments:

Post a Comment