KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 25, 2016

HII SASA SIFA YANGA KAMA ULAYA,YALETA MTENDAJI MKUU WA KLABU KUTOKA UFARANSA.

umuyo

Mfaransa Jerome Dufourg

……………………………………………………………………………………

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.

Timu ya Yanga imeamua kwenda sawa na TP Mazembe,Zamalek na Mamelodi kwa kumuajiri Mfaransa Jerome Dufourg kuwa mtendaji mkuu wa klabu kwa kumpa mkataba wa miaka mitatu na anatarajia kuja Dar kumalizana uongozi na kazi rasmi ataanza Novemba wanajangwani wanasuka safu bora ya maendeleo ya klabu.
Mfaransa huyo aliyewahi kufanya kazi Shirikisho la Soka Rwanda (FERWAFA) na klabu ya FC Talanta ya Daraja la Pili Kenya anatarajiwa kuwasili Dar es Salaam wakati wowote kuanza kazi na ataanza rasmi majukumu hayo Novemba 19.

Mfaransa huyu mwenye umri wa miaka 30 atakuja Dar kumalizana na uongozi uliochini ya Mwenyekiti Manji na Yanga ina malengo ya kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa hivyo imeanza kusuka safu hatari na yenye uweredi na watu wenye mpira ndio maana imemchukua Mfaransa huyu ambaye anaonekana ni mzoefu.
Jukumu la kwanza kubwa la Dufourg na kuhakikisha mapato ya klabu yanazidi matumizi. Mwaka jana Yanga iliingiza Sh Bilioni 1.3 wakati ilitumia Sh Bilioni 2.8.

Yanga ina mpango wa kubadilisha benchi la ufundi lote mpaka sasa wameingia mkataba na kocha wa Zesco United ya Zambia George Lwandamina aliyechukua mikoba ya Pluijm aliyejiuzulu

No comments:

Post a Comment