KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 21, 2016

KAMATI YA MASAA 72 KUTOA HUKUMU YA MASHABIKI WA COASTAL UNION YA KUMPIGA MWAMUZI.

boiplus
Kamati ya masaa 72 inatarajia kukaa kujadili vurugu za mashabiki wa Coastal Union cha kumvamia mwamuzi Thomasi Mkombozi na kumshushia kipigo kama mwizi baada ya kuwapa penati wageni timu ya KMC ya jijini Dar es salaam.
Ripoti hiyo inajadiliwa baada ya kamishni na FA ya mkoa wa Tanga kuwasilisha ripoti hiyo kwa kamati ya mashindano ya TFF.
Hata hivyo kumekuwa na hofu kuwa, huenda Coastal Union inaweza kuondolewa kwenye uwanja huo kutokana na tabia za mashabiki wake kuwapiga waamuzi mara kwa mara hii ni mara ya tatu walifanya hivyo mwakani kwa kufanya vurugu dhidi ya Mbeya City Ligi na Yanga FA.
Kwa upande wa msemaji wa TFF Msemaji, Alfred Lucas, amesema kuwa pamoja na kusubiria maamuzi ya kamati hiyo, kanuni za wazi ni kwamba iwapo ripoti zitabainisha mashabiki ndio wenye makosa, basi Coastal kuna hatari ya kucheza mechi zilizobaki bila mashabiki ama kuhamishwa kutoka uwanjani hapo.
Mchezo huo wa Ligi daraja la kwanza ulimalizika kwa Coastal kulala jumla ya mabao 3-2 na kuendelea kufanya vibaya katika ligi hiyo na ikumbukwe mwaka jana timu za mkoa wa Tanga ziliweka rekodi Duniani kwa kushuka zote tatu ambazo ni Coastal,JKT Mgambo na African Sports.

No comments:

Post a Comment