KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 5, 2016

KMKM YAANDAA MATEMBEZI YA KILOMITA 10 OKTOBA 29

Kikosi cha kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM) kupitia kwa Mwenyekiti wake wa  Kikosi hicho KMKM Sports Club,  Kapteni Khatib Khamis Mwadini amebainisha kuwa,  mbio hio za Kilomita 10  zitakazofanyika tarehe 29 mwezi huu zinatarajia kuanzia Makao Makuu ya kikosi hicho  Kibweni na kumalizikia Uwanaja wa Maisara Mjini Zanzibar.
Na kuongeza kuwa,  tayari maandalizi yanaendelea huku  taratibu zote zikiwa zimesha fuatwa.
0c2Mwenyekiti wa Kikosi cha Kuzuia Magenzo Zanzibar (KMKM) Sports Club Kapteni Khatib Khamis Mwadini akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu mbio za Kilomita 10  zitakazofanyika tarehe 29 mwezi huu kuanzia Makao Makuu ya kikosi hicho  Kibweni na kumalizikia Uwanaja wa Maisara Mjini Zanzibar.
0ww3Mwenyekiti wa Chama cha riadha Zanzibar Abdulhakim Cosmas akitoa maelekezo juu ya mbio za Kilomita 10 zilizoandaliwa na Kikosi cha KMKM katika Mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Makao Makuu ya Kikosi hicho Kibweni.
05Mwenyekiti wa Kamati ya ufundi wa mbio za Kilomita 10 za KMKM Luteni Mlingi Mganga Bwire akijibu maswala yaliyoulizwa na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Kikosi hicho Kibweni Mjini Zanzibar.
kmkmMwenyekiti wa Kikosi cha Kuzuia Magenzo Zanzibar (KMKM) Sports Club Kapteni Khatib Khamis Mwadini akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (Hawapo pichani).
Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar

No comments:

Post a Comment