KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 24, 2016

MATEKA WASEMA WALIKULA PANYA SOMALIA

Mateka walioachiliwa huru baada ya kuwasili Kenya, 23 Oktoba 2016.
Mateka hao waliachiliwa huru wikendi na wakafika Kenya Jumapili.
Kundi la mabaharia ambao waliachiliwa huru Jumamosi baada ya kuzuiliwa na maharamia kwa miaka mitano nchini Somalia walikula hata panya ili waishi, mmoja wao ameambia BBC.
Arnel Balbero, kutoka Ufilipino amesema walikuwa wanapewa maji kidogo sana na walijihisi kama "wafu waliokuwa wakitembea" kufikia wakati wa kuachiliwa huru kwao.
Mabaharia hao walitekwa wakiwa kwenye meli mwaka 2012 kwenye pwani ya Ushelisheli na wakapelekwa Somalia bara na kuzuiliwa mateka.
Waliachiliwa huru Jumamosi. Taarifa zinasema waliokuwa wanawazuilia mateka walilipwa kikombozi.BBC

No comments:

Post a Comment