Rais Dk. John Pombwe Magufuli
akizungumza Ikulu jana kuhusu mgeni wake Mfalme Mohammed VI
anayemsikiliza kukubali kujenga uwanja mkubwa wa michezo mkoani Dodoma
pamoja na msikiti mkubwa jijini Dar es salaam a ukiacha mikataba zaidi
ya 20 ya kibiashara iliyosainiwa jana kati ya makampuni ya Tanzania na
Morocco Ikulu jijini Dar es salaam.
(PICHA NA HASSAN SILAYO -MAELEZO)
……………………………………………………………….
Na Daudi Manongi; MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli amesema kuwa wamekubaliana na Mfalme
Mohamed wa Sita wa Morocco kujenga Uwanja wa Mpira wa miguu wa kisasa
mkoani Dodoma utakaogharimu dola milioni 100.
Rais Magufuli ameyasema hayo leo
Ikulu Jijini Dar es Salaam baada ya kutiliana saini kwa mikataba 21 ya
makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi za Tanzania na Morocco.
“Mbali na mikataba baina ya
Tanzania na Morocco nimezungumza mambo mbalimbali na Mfalme Mohamed wa
Sita wa Morocco na nimemuomba atujengee Uwanja mkubwa wa mpira pale
Makao Makuu yetu Dodoma utakaokuwa na thamani kati ya dola milioni 80
hadi 100 na amesema ataujenga, kwa hiyo utakuwa Uwanja mkubwa kuliko wa
Dar es Salaam”. Alisema Rais Magufuli.
Mbali na hayo Rais Magufuli
amewahakikishia wafanyabiashara wa Morocco kuwa Tanzania ni salama na
inapenda kushirikiana nao, na kuwa nchi yetu iko katika mwelekeo mzuri
wa uwekezaji ambapo uchumi wa nchi yetu unategemea kukua kwa asilimia
7.2 mwishoni mwa mwaka.
Kwa upande wake Waziri wa Mambo
ya Nje wa Morocco Bw.Salahddine Mezour ameishukuru nchi ya Tanzania kwa
ushirikiano iliounyesha na kusema kuwa Morocco itaendelea kushirikiana
na Tanzania katika Nyanja mbalimbali kwa kuwa ina utulivu wa kisiasa na
icho ndo kimekuwa kivutio kikubwa katika kuwekeza kwao nchini hapa.
Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco
yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais, Dk
John Pombe Magufuli ikiwa na lengo la kuimarisha uhusiano uliopo baina
ya nchi hizi mbili na kutiliana saini mikataba 21 ya makubaliano ya
ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
No comments:
Post a Comment