
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akifungua
kongamano la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini Oktoba 18,
2016 jijini Dar es salaam wakati wa wiki ya maadhimisho ya Umoja wa
Mataifa unaofikisha miaka 71 tangu kuasisiwa kwake. Maadhimisho ya hayo
yanaongozwa na kaulimbiu kwa upande wa Tanzania inayosema “Jukumu la
Vijana wa Tanzania katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii”.

Mwakilishi wa Shirika Umoja wa
Mataifa nchini linaloshughulikia Maendeleo (UNDP) Annamaria Kiaga
akimkaribisha Mgeni Rasmi ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel kufungua
kongamano la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini Oktoba 18,
2016 jijini Dar es salaam

Baadhi ya washiriki wa kongamano
la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini wakimsikiliza Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole
Gabriel Oktoba 18, 2016 jijini Dar es salaam wakati wa ufunguzi wa
kongamano la vijana lililoandaliwa na Shirika Umoja wa Mataifa
linalishughulikia Maendeleo (UNDP).

Baadhi ya washiriki wa kongamano
la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini wakimsikiliza Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole
Gabriel Oktoba 18, 2016 jijini Dar es salaam wakati wa ufunguzi wa
kongamano la vijana lililoandaliwa na Shirika Umoja wa Mataifa
linalishughulikia Maendeleo (UNDP).

…………………………………………………………………..
Na Eleuteri Mangi, WHUSM
Mataifa wanachama wa Umoja wa
Mataifa (UN) yanashiriki kwenye shughuli mbalimbali za kijamii kuelekea
kilele cha maadhimisho ya miaka 71 ya umoja huo kinachofikia Oktoba 24
mwaka huu baada ya kuasisiwa kwake mwaka 1945.
Tanzania ambayo ni mwanachama hai
wa UN imeungana na umoja huo kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali
za kuunganisha nguvu za vijana na kuwajenga kimaadili, kiuchumi ili
waweze kujitambua na kujua mustakabali wao katika kujenga uchumi wa
nchi.
Kwa kuwa vijana ni nguzo kuu ya
kujenga taifa lolote duniani, Tanzania kwa kukushirikiana Umoja wa
Mataifa imeona umuhimu wa kuwashirikisha vijana kupitia kongamano la
vijana kutoka shule za sekondari na vyuo vikuu nchini lililofanyika
Oktoba 18 mwaka huu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu
Julius Nyerere (JNICC) uliopo jijini Dar es salaam.
Lengo la kongamano hilo ni
kuwashirikisha vijana kujadili namna watakavyoshiriki katika kutekeleza
Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) na kutafuta namna bora ya kutatua
changamoto zinazowakabili vijana nchini.
Vijana hao wamepata fursa ya
kukumbushana, kuelimishana na kubadilishana mawazo juu ya namna bora
inayowawezesha kutoa mchango wao katika masuala ya kiuchumi na maendeleo
ya kijamii nchini.
Kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya
Maendeleo ya Viana ya mwaka 2007, ujana ni kundi mtambuka ambalo
linajumuisha vijana kuanzia miaka 15 hadi 35 ndio maana wanaitwa ni
nguvu kazi ya taifa kwa kuwa wengi wao kuanzia miaka 18, umri wa mtu
mwenye nguvu na uwezo mzuri wa kufikiri na kuchangia katika maendeleo ya
taifa kiuchumi na kijamii.
Akifungua kongamano hilo, Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole
Gabriel amewaasa vijana kuwa watakumbukwa kwa mchango wao watakaotoa
kwa jamii na si kwa nafasi zao kwa kuchangia uchumi na maendeleo ya
nchi, hivyo ni wajibu watambue umuhimu wao kwa taifa.


No comments:
Post a Comment