Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.
Mrisho Gambo (kwanza kulia) akizungumza na wananchi wa Kata ya Terrati
kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya Msingi
Mkonoo.
Baadhi ya wananchi wa Kata ya Terrati waliohudhuria Mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Ndg.
Athumani Kihamia (aliyesimama) akiwatambulisha wakuu wa Idara za Jiji
(hawapo Pichani) kwenye Mkutano wa hadahara.
Mhandisi wa barabara Jiji la
Arusha Fordia Mwankenja (anayepunga mkono) akiwasalimia wananchi wa Kata
ya Terrari kwenye Mkutano wa hadhara
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe.
Fabian Gabriel Daqarro akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuzungumza
na wananchi wa Kata ya Terrati kwenye Mkutano wa hadhara.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Ilaitayoki
Mhe. Long’ida Lomayani Kupitia Chadema akiwasilisha kero za mtaa wake
kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha
……………………………………………………………………………
Nteghenjwa Hosseah – Arusha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.
Mrisho Mashaka Gambo amechangia Lita 600 za mafuta kwa ajili ya greda la
Halmashauri ili liweze kutengeneza miundombinu ya barabara kwenye
maeneo yote korofi yanayozunguka kata ya Terrati.
Rc Gambo amefanya hivyo wakati wa
mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata ya Terrat uliofanyika kwenye
Shule ya Msingi Terrat wenye lengo la kufahamu changamoto za muda muda
mrefu zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.
Katika Mkutano huo Mkuu wa Mkoa
alianadamana na watalaamu wa Taasisi mbalimbali zinazotoa huduma katika
Mkoa huu pamoja na menegiment ya Jiji ili kuwezesha upatikanaji wa
majawabu ya kero zote zilizo wasilishwa na wananchi hao ikiwa ni pamoja
na utekelezaji wa haraka ili kumaliza kabisa changamoto hizo.
Wananchi wa Kata hiyo wamesema
kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na kero ya ubovu wa miundombinu ya
barabara, kukosekana kwa maji safi na salama pamoja na umeme katika
eneo hilo na pia walitoa shukrani zao kwa Mkuu wa Mkoa kwa kuwapa
kipaumbele katika ziara zake za kutambua changamoto za Mkoa wake.
Sisi wakazi wa huku tumekua kama
hatuishi kwenye Jiji la Arusha kwa sababu huduma zote muhimu zimekuwa
kikwazo sana kwetu mpaka zinasababisha kudorora kwa uchumi kwa wakazi
wa maeneo haya kwa kuwa hapavutii wafanyabiashara kuja kuwekeza wala
wanunuzi kutoka mjini hivyo tumekua tukiuziana sisi kwa sisi ambao wote
tuna vipato duni alisema Jumanne Juma Kingu.
Mmoja wa wananchi hao
aliyejitambulisha kwa Jina la Eliakim Mason kutoka Mtaa wa bondeni kati
alisema kuwa Gari lakubebea wagonjwa katika kituo cha Afya Mkonoo
limeharibika kwa kipindi kirefu sana na wanapata tabu ya kusafirisha
mgonjwa hadi kufikia kwenye Hospital za Mjini Arusha inawalazimu kukodi
Gari kwa gharama kubwa ili kunusuru maisha ya ndugu zao pia alilalamikia
uhaba wa watumishi katika Kituo cha Afya Mkonoo na kudai kwamba inakuwa
vigumu kupata hudma bora wagonjwa wanapokua wengi katika kituo hicho.
Akitoa majibu ya malalamiko hayo
Mkuu wa Mkoa wa Arusha alisema changamoto hizi zimekuwa za kipindi
kirefu lakin hivi sasa zimefika mwisho kwa sababu Serikali ya Awamu ya
Tano ni ya kutatua kero na vitendo ndivyo vinavyotawala hivyo ndani ya
muda mfupi eneo hili litakua sehemu nzuri ya kuishi kwa kuwa kero hizi
zitakuwa historia.
Rc Gambo alimuagiza Maneja wa
Tanesco Mkoa kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa Kata ya Tarati
ndani ya miezi mitatu pia aliwataka viongozi wengine wa Taasisi
zinazolalamikiwa kutolea ufafanuzi na mikakati ya haraka ya kumaliza
kabisa matatizo ya wananchi wa Terrat.
Naye Mkurugenzi wa Jiji la Arusha
Ndg. Athumani Kihamia aliahidi mbele ya Mkutano huo kwamba ndani ya
wiki mbili gari la kubebea wagonjwa kwenye Kituo cha Afya Mkonoo
litakuwa limeshatengenezwa na kuanza kutoa huduma na pia ataongeza
watumishi wa kutosha ili kuboresha utoaji wa huduma za Afya katika Kituo
hicho.
Eng. Ruth Koya ni Mkuu wa Idara
ya Maji safi na maji Taka (AUWSA) alieleza kuwa Taasisi yake imeanza
kutekeleza mradi mkubwa wa uboreshaji wa miundombinu pamoja na
upatikanaji wa maji safi na salama na Kata ya Terrati ni miongoni mwa
maeneo ambayo yatafikiwa na mradi huo na utamaliza kabisa changamoto hii
ya maji.
Mkutano huu ulihudhuriwa na
wananchi wa chama cha demokrasia na maendeleo akiwemo Mwenyekiti wa Mtaa
wa Ilaitayok Mhe. Long’ida Lomayani.
No comments:
Post a Comment