Wakicheza katika uwanja wa Cristal Arena nchini Ubelgiji wenyeji KRC Genk imepata ushindi wa pili michuano ya kombe la Europa baada ya kuwahenyesha Athletic Bilbao jumla ya mabao 2-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa
Genk kufanya mabadiliko kwa kumtoa Thomas Buffel na nafasi yake
kuchukuliwa na Mtanzania Mbwana Samatta dakika ya 56 kuingia kwa Samatta
kulileta uhai tena katika safu ya ushambuliaji.
Samatta alionesha kuwa yeye sio
mtu wa mchezo kwa kusababisha bao la pili dakika ya 84 likifungwa na
Onyinye Ndidi kwa shuti kali lililoenda moja kwa moja na kuwafanya
Bilbao kutoka nje kwa huzuni hadi mwamuzi Stefan Johannesson anamaliza
mpira Genk wameibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Kwa matokeo hayo Genk
wanashikilia usukani mwa msimamo wa kundi F wakiwa na alama 6 wakati
Bilbao wana alama 3 na kushika nafasi ya mwisho na Rapid Vienna na
Sassuolo zote zikiwa na alama 4 baada ya kutoka sare ya kufungana bao
1-1,timu hizi zitarudiana Novemba 3 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment