KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 26, 2016

SERIKALI YAZITAKA NGO ZA ELIMU YA UKIMWI KUSITISHA HUDUMA HIYO

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeagiza taasisi na mashirika yote yasiyo ya kiserikali (NGO’s) yanayohusika na utoaji wa elimu ya Ukimwi kusitisha huduma hizo hadi itakapo toa muongozo mpya wa utoaji huduma katika ngazi ya jamii.
Waziri wa Wizara ya Afya, Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, alisema kumekuwepo na ongezeko kubwa la NGO’s ambazo zinasababisha muingiliano katika utoaji huduma za kijamii pamoja na kufanya kazi katika mikoa michache, ambapo amemuagiza Mganga Mkuu wa Serikali kuzipangia mikoa taasisi zinazotaka kufanya kazi.
“Serikali inaendelea kuzuia utolewaji wa huduma hizo kwa ngazi ya jamii hadi pale ambapo wizara itapitia mwongozo mpya wa utoaji huduma ngazi za kijamii kwa makundi maalumu. Shughuli za NGO’s kwenda kwa jamii kugawa vilainishi au kutoa elimu zitasimama hadi itakapotolewa mwongozo mpya wa utoaji huduma kwa jamii,” alisema.
Amesema wizara imeweka utaratibu mpya wa kusajili taasisi hizo na kwamba kabla ya kuanza kufanya kazi zinatakiwa kutoa taarifa kwa mkurugenzi wa halmashauri anayotaka kufanyia kazi.
“Kumekuwepo na ongezeko kubwa la idadi ya wadau wanaohitaji kusaidia serikali, ili kuleta huduma hizo kwa ngazi ya jamii, na kwamba ili kuleta tija, uwajibikaji na uwazi katika utolewaji wa huduma hizo, mganga mkuu wa serikali atawapanga wadau katika mikoa kulingana na idadi yao,” alisema.
Amesema NGO’s hizo zinatakiwa kutambuliwa na halmashauri husika kabla ya kuanza kazi.
“Mkurugenzi wa halmashauri atatambulisha wadau au NGOs na kutia kibali, tunazuia asasi hizi kutoka nje ya mkoa wa Dar es Salaam kufanya kazi pasipo kuthibitishwa na wamurugenzi wa halmashauri,” alisema.
Kutasainiwa makubaliano ya kufanya kazi kusudi muweke makubaliano ya namna ya ufanyaji kazi. Lengo letu kumsaidia waziri wa katiba na sheria, hatutaki watu kuitumia wizara ya afya kukiuka sheria kwa kigezo cha kusaidia jamii.

No comments:

Post a Comment