Katika
mkakati wake wa kufanya uwekezaji wa mitambo inayotumia teknolojia ya
kisasa na kufanya uzalishaji usiochafua mazingira,kampuni ya TBL Group
imeanza kufanya uzalishaji wa bia kwa kutumia umeme unaotokana na
nishati ya jua.
Uzalishaji
wa kutumia umeme wa jua umeanza mapema wiki hii katika kiwanda cha bia
cha Mbeya baada ya kukamilika kwa zoezi la kufunga vifaa vya kuvuna
umeme wa jua kwenye kiwanda hicho vyenye uwezo wa kuzalisha umeme wa
kilowati 138.
Mkurugenzi
wa ufundi wa kampuni hiyo,Gavin Van Wijk, amesema kuwa teknolojia ya
matumizi ya umeme unaotokana na nishati ya jua kuendesha kiwanda kikubwa
kama hicho ni mpya hapa nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Alisema
mitambo hiyo ya umeme wa jua imetengenezwa nchini Ujerumani na ina
uwezo wa kuzalisha Kilowatt 138 na inao uwezo wa kukidhi mahitaji ya
matumizi ya umeme wa kiwanda kwa asilimia zaidi ya 30%.
No comments:
Post a Comment