Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA) Bw. Alphayo Kidata – (Mwenye
suti ya bluu katikati) pamoja na Kamishna wa Kodi za Ndani TRA Bw.
Elijah Mwandumbya (Kushoto kwake) wakiwa katika picha ya pamoja na
walipakodi waliofika katika Ofisi Mpya ya TRA Kimara ili kuhakiki Namba
zao za Utambulisho wa Mlipakodi –TIN. Ofisi hiyo imezinduliwa leo tarehe
26 Oktoba 2016 na Kamishna Mkuu wa TRA ili kuwafikia wananchi kwa
karibu zaidi na kuboresha huduma mbalimbali za Kodi.
Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA) Bw. Alphayo Kidata akikata
utepe kama ishara rasmi ya uzinduzi wa ofisi mpya ya TRA iliyoko Kimara
Mwisho leo Tarehe 26 Oktoba 2016, Kushoto kwake ni Kamishna wa Kodi za
Ndani TRA Bw. Elijah Mwandumbya pamoja na Wakurugenzi wengine wa TRA
wakishuhudia tukio hilo
Meneja
wa TRA Kinondoni Bw. Wallace Mnkande (anayeongea kwa vitendo) akitoa
maelezo ya kituo hicho kipya kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (aliyeketi) wakati wa uzinduzi wa
ofisi hiyo. Wengine kutoka kulia ni Kamishna wa Kodi za Ndani TRA Bw.
Elijah Mwandumbya, Naibu Kamishna wa Kodi za Ndani Bw. Abdul Zuberi,
Meneja wa Majengo Gerald Mwikuka, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Bw.
Gerald Mwanilwa na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw.
Richard Kayombo.
:Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA) Bw. Alphayo Kidata
akisalimiana na baadhi ya walipakodi waliofika katika ofisi mpya ya TRA
iliyoko eneo la Kimara Mwisho ili kuhakiki Namba zao za Utambulisho wa
Mlipakodi –TIN wakati wa uzinduzi wa ofisi hiyo.
Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA) Bw. Alphayo Kidata akiongea
na baadhi ya walipakodi waliofika katika ofisi mpya ya TRA-Kimara
Mwisho ili kuhakiki Namba zao za Utambulisho wa Mlipakodi –TIN wakati wa
uzinduzi wa ofisi hiyo.
Kamishna
wa Kodi za Ndani TRA Bw. Elijah Mwandumbya akimweleza jambo Kamishna
Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata alipotembelea ofisi mpya za TRA Kimara
Mwisho kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa ofisi hiyo.
Meneja
wa TRA Kinondoni Bw. Wallace Mnkande akimwonesha jambo Kamishna Mkuu wa
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kushoto kwake)
alipotembelea ofisi ya TRA Kimara Mwisho wakati wa uzinduzi huo
uliofanyika tarehe 26 Oktoba 2016
…………………………………………………………
Katika jitihada za kuboresha
huduma kwa walipakodi na kuzifikisha huduma hizo kwa karibu zaidi
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA) Bw. Alphayo Kidata
amezindua ofisi mpya ya TRA katika eneo la Kimara Mwisho jijini Dar es
Salaam Tarehe 26 Oktoba 2016 itakayotoa huduma zote za kikodi ikiwemo
usajili na uhakiki wa Namba za Utambulisho wa Mlipakodi –TIN, Usajili
wa Kodi ya Ongezeko la Thamani-VAT, Malipo ya Kodi za Magari, Kodi zote
za Mapato zikiwemo Kodi za Makampuni, Watu Binafsi, Wafanyakazi (PAYE),
Kuendeleza Ufundi Stadi – SDL, VAT, Ushuru wa Stampu na huduma nyingine
za kikodi.
Akizungumza na walipakodi
waliofika katika ofisi hiyo kupata huduma wakati wa uzinduzi, Bw. Kidata
aliwashukuru kwa mwitikio wao katika zoezi la uhakiki wa taarifa za TIN
ambao utaisaidia Mamlaka kupata idadi sahihi ya walipakodi ili kuondoa
walipakodi hewa ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za ulipaji kodi.
“Zoezi hili litaongeza ufanisi katika suala zima la usimamizi na ukusanyaji kodi kwa kiwango cha juu” Alisema Bw. Kidata
Kamishna Mkuu wa TRA aliwataka
walipakodi hao wanaoishi maeneo ya karibu na ofisi hiyo mpya ya TRA
iliyopo Kimara Mwisho kuendelea kujitokeza kwa wingi ili kupata huduma
mbalimbali za kikodi ikiwemo uhakiki wa taarifa zao TIN kabla ya tarehe
ya mwisho wa zoezi hilo kwa Mkoa wa Dar es Salaam ambayo ni tarehe 30
Novemba 2016.
Aidha Kamishna wa Kodi za Ndani
TRA Bw. Elijah Mwandumbya alisema TRA imejipanga kuhakikisha inaendelea
kuboresha huduma zake na kuwafikia walipakodi kwa ukaribu zaidi ili
kuondoa usumbufu na kuokoa muda wa upatikanaji wa huduma hizo.
“TRA kwa kuhakikisha
walipakodi wanapata huduma iliyo bora imeanzisha vituo vingi vya kodi
katika jiji la Dar es Salaam na nchi nzima ili walipakodi wapate
huduma stahiki na ya haki na kuiwezesha Serikali kupata mapato yake kwa
mendeleo ya Taifa letu” Alisema Bw. Mwandubya.
No comments:
Post a Comment