KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 15, 2016

TUNAENDELEA KUZIBA MIANYA YA RUSHWA/WAFICHUENI WAFUJA FEDHA ZA SERIKALI

mla1
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MAKAMU wa rais ,Samia Suluhu Hassan,amewataka kuwafichua watumishi mbalimbali wa halmashauri na taasisi za serikali katika wilaya na mikoa wanaodhaniwa kufuja fedha za serikali na kupoteza mapato lengo ikiwa ni kuzikusanya fedha na kuzirudisha katika mikono ya wananchi waone faida yake.
Amesema serikali ya awamu ya tano inaendelea na nguvu yake ya kukusanya mapato na kuziba mianya ya rushwa na kupotea kwa mapato na amewasisitiza wananchi kulipa kodi pale inapohitajika ili kusaidia na serikali kuinua mapato yake.
Aidha Samia ametoa rai kwa wananchi mkoani Pwani kuenelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kulinda  amani na usalama wa mkoa huo kufuatia  kujitokeza kwa mambo ambayo yameonekana kuhatarisha usalama wa mkoa hivi karibuni.
Katika hatua nyingine amewahakikishia wakazi wa mji wa Chalinze kutatua tatizo la maji ambalo bado ni kero kubwa ambapo ameeleza kwamba mwishoni mwa mwaka huu matunda yataanza kuonekana.
Akizungumza na baadhi ya wananchi wa Mlandizi na Chalinze,mkoani Pwani wakati aliposimama kuwasalimia akielekea mjini Dodoma kikazi,alisema wananchi waiamini serikali yao kwani imeanza kuirejesha nchi katika nidhamu ya mapato na matumizi na kazi ya maendeleo inaendelea.
“Watanzania watajenga Tanzania yao wenyewe na serikali yake na Tanzania inaweza kujiendesha yenyewe na kama itategemea misaada iwe sio kwa kiasi kikubwa.”alisema.
Hata hivyo Samia aliwataka wakulima na wafugaji kuishi kwa upendo na mshikamano baina yao pasipo kutofautiana kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha migogoro isiyo na tija na wakati mwingine kuvunja amani.
Kufuatia ombi la mbunge wa jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete ,kumeelezea kuhusu kero ya maji inayowakabili wakazi wa jimbo hilo,Samia alisema serikali inatambua hilo na kwasasa ipo katika mpango mzuri wa kumaliza tatizo la maji lililopo.
Alielezea kuwa WAMI yapo maji ya kutosha lakini tatizo ni usambazaji ,hivyo wanatarajia kuvuta maji kwa mabomba hadi eneo la Pera na kujenga matanki makubwa yenye ujazo wa lita 300,000 ,Kibiki watajenga tanki lenye ujazo wa lita 200,000 ili maji yakifungwa kuweze kuwa  na maji ya kufikisha kwa wananchi kirahisi.
Makamu huyo wa rais alisema watajenga hifadhi nyingine ya maji pale Mazizi yenye lita mil.2 ambayo itawezesha kutumia maji ndani ya wiki mbili bila kukatika ambapo mpango huo upo njia na tayari mkandarasi yupo na wametanguliza sh.bil 43 ili kazi ianze .
Samia wakati anafanya kampeni ili kuomba kuchagulia kuingia madarakani aliahidi kuwatua akinamama ndoo kichwani kwa kutatua tatizo la maji na kusema anashughulikia suala hilo hadi hapo atakapowaondolea wananachi adha ya kutembea umbali mrefu kusaka huduma hiyo muhimu.

No comments:

Post a Comment