
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MAKAMU wa rais ,Samia Suluhu
Hassan,amewataka kuwafichua watumishi mbalimbali wa halmashauri na
taasisi za serikali katika wilaya na mikoa wanaodhaniwa kufuja fedha za
serikali na kupoteza mapato lengo ikiwa ni kuzikusanya fedha na
kuzirudisha katika mikono ya wananchi waone faida yake.
Amesema serikali ya awamu ya tano
inaendelea na nguvu yake ya kukusanya mapato na kuziba mianya ya rushwa
na kupotea kwa mapato na amewasisitiza wananchi kulipa kodi pale
inapohitajika ili kusaidia na serikali kuinua mapato yake.
Aidha Samia ametoa rai kwa
wananchi mkoani Pwani kuenelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na
usalama kulinda amani na usalama wa mkoa huo kufuatia kujitokeza kwa
mambo ambayo yameonekana kuhatarisha usalama wa mkoa hivi karibuni.
Katika hatua nyingine
amewahakikishia wakazi wa mji wa Chalinze kutatua tatizo la maji ambalo
bado ni kero kubwa ambapo ameeleza kwamba mwishoni mwa mwaka huu matunda
yataanza kuonekana.
Akizungumza na baadhi ya wananchi
wa Mlandizi na Chalinze,mkoani Pwani wakati aliposimama kuwasalimia
akielekea mjini Dodoma kikazi,alisema wananchi waiamini serikali yao
kwani imeanza kuirejesha nchi katika nidhamu ya mapato na matumizi na
kazi ya maendeleo inaendelea.
“Watanzania watajenga Tanzania
yao wenyewe na serikali yake na Tanzania inaweza kujiendesha yenyewe na
kama itategemea misaada iwe sio kwa kiasi kikubwa.”alisema.
Hata hivyo Samia aliwataka
wakulima na wafugaji kuishi kwa upendo na mshikamano baina yao pasipo
kutofautiana kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha migogoro isiyo na
tija na wakati mwingine kuvunja amani.
Kufuatia ombi la mbunge wa jimbo
la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete ,kumeelezea kuhusu kero ya maji
inayowakabili wakazi wa jimbo hilo,Samia alisema serikali inatambua hilo
na kwasasa ipo katika mpango mzuri wa kumaliza tatizo la maji lililopo.
Alielezea kuwa WAMI yapo maji ya
kutosha lakini tatizo ni usambazaji ,hivyo wanatarajia kuvuta maji kwa
mabomba hadi eneo la Pera na kujenga matanki makubwa yenye ujazo wa lita
300,000 ,Kibiki watajenga tanki lenye ujazo wa lita 200,000 ili maji
yakifungwa kuweze kuwa na maji ya kufikisha kwa wananchi kirahisi.
Makamu huyo wa rais alisema
watajenga hifadhi nyingine ya maji pale Mazizi yenye lita mil.2 ambayo
itawezesha kutumia maji ndani ya wiki mbili bila kukatika ambapo mpango
huo upo njia na tayari mkandarasi yupo na wametanguliza sh.bil 43 ili
kazi ianze .
Samia wakati anafanya kampeni ili
kuomba kuchagulia kuingia madarakani aliahidi kuwatua akinamama ndoo
kichwani kwa kutatua tatizo la maji na kusema anashughulikia suala hilo
hadi hapo atakapowaondolea wananachi adha ya kutembea umbali mrefu
kusaka huduma hiyo muhimu.


No comments:
Post a Comment