Mkurugenzi wa mawasiliano wa taasisi ya
Mfuko wa Wanawake Afrika, Anna Salado (kulia), akipakua mboga zilizopikwa
kiasili na kuungwa kwa nazi wakati yeye na ujumbe wake walipotembelea mradi wa
ukaushaji wa mboga na matunda wa wanawake wa Kata ya Mzinga mkoani Morogoro
hivi karibuni. Kushoto
ni Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro, Milikieli Mansweat Mahiku.
Mratibu wa mradi wa Green Voices kutoka
taasisi ya Mfuko wa Wanawake Afrika ya Hispania, Alicia Cebada, akiwa
ameshikilia pakiti ya kisamvu kilichokaushwa na kufungashwa huku akiwapongeza
wanawake wa kikundi cha Mzinga katika Kata ya Mzinga, Manispaa ya Morogoro
kwamba wamefanya kazi nzuri sana. Mwenye fulana nyeupe ni Bi. Esther Muffui,
mshiriki kiongozi wa mradi huo.




No comments:
Post a Comment