Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameuagiza
Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kuboresha Idara ya Mipango na
Usanifu katika wakala huo ili kupata matokeo mazuri katika utekelezaji
wa miradi mbalimbali nchini.
Prof.
Mbarawa ameutaka wakala huo kuboresha kanuni zinazosimamia aina ya
vyombo vya moto vinavyotumia barabara zote nchini ikiwemo ili kuweza
kusaidia miundombinu hiyo kudumu muda mrefu.
Akizungumza
mkoani Dodoma katika ufunguzi wa Baraza la Saba la Wafanyakazi wa
Wakala huo Prof. Mbarawa amesema kuwa wakala unabidi uanze kubadili aina
ya mfumo wa usanifu uliokuwa ukitumika awali na badala yake utumike
usanifu wa kisasa unaoendana na mahitaji halisi ya watumiaji wa barabara
hizo.
![]() |
| Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza
na wajumbe katika Baraza la Saba la Wafanyakazi wa Wakala wa Barabara
nchini (TANROADS), lililofanyika mkoani Dodoma.
“Kama
mnaona kuna mabadiliko yoyote mnayohitaji kuyafanya ili barabara zetu
zidumu, boresheni kanuni na mlete kwangu ili nizifanyie kazi”, amesema
Waziri Prof. Mbarawa.
Ameongeza
kuwa katika kuboresha utendaji katika wakala huo, Serikali ina mpango
wa kuwapa fursa za ajira wahandisi hususani wanawake ili na kuwajengea
uwezo na kuweka uwiano katika taalamu hiyo.
Aidha
Waziri Prof. Mbarawa ameahidi kuongeza fedha za uendeshaji kwa wakala
huo ili kuuwezesha kutekeleza miradi mbalimbali inayoendelea nchini.
“Kumbukeni
majukumu ya Wakala yameongezeka sasa hamtajenga barabara pekee,
mmeongezewa jukumu la kujenga miundombinu ya viwanja vya ndege hivyo ni
muhimu kujipanga kutekeleza kazi hii”, amesisitiza Prof. Mbarawa.
|
![]() |
| Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale
ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Saba la Wafanyakazi akitoa taarifa ya
utendaji kazi wa Wakala huo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani). Baraza hilo
limefanyika mkoani Dodoma.
Naye,
Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Patrick Mfugale ameahidi kushughulikia
ujenzi wa viwanja vya ndege ikiwemo kufanya kazi kwa weledi na uadilifu
kama ambavyo wakala huo unatekeleza miradi yake ya barabara.
Ameongeza
kuwa Wakala unaendelea kufanya kazi na Makandarasi wenye uwezo na
wanaozingatia thamani ya fedha katika miradi yote inayotekelezwa nchini.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya TANROADS, Eng. Hawa Mmanga amemuahidi
Waziri Prof. Mbarawa kufanya kazi kwa uadilifu, bidii, na kuzingatia
thamani ya fedha katika miradi yote inayotekelezwa na wakala.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
|
![]() |
| Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Saba la Wafanyakazi wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani), katika Baraza hilo. |
![]() |
| Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa katika Baraza la Saba la Wafanyakazi wa Wakala huo lililofanyika mkoani Dodoma. |
![]() |
| Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Saba la Wafanyakazi wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS). |
![]() |
| Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akimsikiliza mmoja wa wajumbe waliohudhuria katika Baraza la Saba la Wafanyakazi wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoani Dodoma. |








No comments:
Post a Comment