KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 8, 2016

WAZIRI MWAKYEMBE AMPONGEZA BALOZI WA VIETNAM

viet
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria, Dkt. Harrison Mwakyembe, amempongeza Balozi Vo Than Nam wa Vietnam anayemaliza kipindi chake nchini, kwa mchango wake mkubwa katika kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi kati ya Vietnam na Tanzania.
  Dkt Mwakyembe alitoa pongezi hizo kwenye hafla ya kuadhimisha miaka 71 ya uhuru wa Vietnam iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam jana jioni. Dkt Mwakyembe  alisema uwekezaji mkubwa uliofanywa na kampuni ya Vietnam ya Halotel katika sekta ya mawasiliano ni moja ya mafanikio makubwa ya mahusiano ya nchi mbili hizi.
  Amesema milango iko wazi kwa makampuni zaidi kutoka Vietnam kuwekeza chini katika sekta mbalimbali na kuongeza kuwa uzoefu ambao Vietnam imeupata katika mageuzi yake ya uchumi kutoka uchumi wa kilimo hadi wa viwanda ni chachu kwa Tanzania inayofuata njia hiyohiyo.
Akimkaribisha Waziri huyo aliyekuwa Mgeni Rasmi kwenye hafla hiyo, Balozi Vo Than Man aliwasifu Watanzania kwa moyo wa ushirikiano na kuahidi kuendeleza mahusiano kati ya nchi hizo

No comments:

Post a Comment