KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 8, 2016

MAADHIMISHO YA SIKU YA POSTA DUNIANI 2016, MKOA WA MWANZA WANG’ARA KWENYE SHINDANO LA UANDISHI WA BARUA KITAIFA.

Meneja wa Shirika la Posta mkoani Mwanza, Julius Chifungo, akizunguza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani ambayo kimkoa yamefanyika leo katika Shule ya Saint Mary’s Seminary (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza.
 
Siku ya Posta duniani huadhimishwa ifikapo Oktoba 09 kila Mwaka ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya Siku ya kuanzishwa kwa Umoja wa Posta Duniani ulioanzishwa mwaka 1874 katika mji wa Berne nchini Switzerland ukijumuisha mataifa 192 duniani.
Na BMG
 
Maadhimisho hayo yamekwenda sambamba na zoezi la kukabidhi zawadi kwa Washindi wa Uandishi wa barua Kitaifa kutoka mkoani Mwanza ambapo washindi watano kati ya 10 bora kitaifa wametoka Saint Mary’s Seminary (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza.
 
Washindi hao na nambari walizoshika kwenye mabano ni, Denis Bahati Stephen (01), Samwel Lufungulo Somelo (02), Vitalis Aloo Awasi (03), Kizito Eliakimu Paschal (04) na Fredrick Elias Mayunga (08).
 
Washindi wa Tano na Sita wametoka Shule ya Mazinde Juu mkoani Tanga, Mshindi wa Saba ametoka Shule ya Lugalo mkoani Iringa, huku Washindi wa Tisa na 10 pia wakitoka Shule ya Mazinde Juu mkoani Tanga.
 
Meneja wa Posta mkoani Mwanza, Julius Chifungo amesema shindano la uandishi wa barua huwashirikisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wasiozidi umri wa miaka 15 ambapo shule za msingi lugha ya kiswahili na kiingereza hutumika na kiingereza pekee kwa shule za sekondari. 
 
Amebainisha kwamba wanafunzi huandika barua yenye mane kati ya 500 na 1,000 kulingana na mada iliyotolewa na kwamba mwaka huu mada ilikuwa ni “Jiandikie barua ukiwa na miaka 45” ambapo barua ya mshindi wa kwanza itakwenda kushindanishwa na barua za washindi wengine kutoka nchi 191 wanachama wa Umoja wa Posta Duniani ambapo mshindi wa kwanza nchini ataliwakilisha taifa kwenye shindalo hilo nchini Switzerland.
Katibu Mtendaji wa Idara ya Elimu, Jimbo Kuu la Mwanza, Alex Masasi, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo akizungumza ambapo amewahimiza wanafunzi kuongeza bidii katika masomo yao hususani kuwa bora kwenye kusoma, kuandika na kuzungumza lugha nyingi tofauti na kiswahili na kiingereza.
Wanafunzi wakimsikiliza kwa umakini Katibu Mtendaji wa Idara ya Elimu, Jimbo Kuu la Mwanza, Alex Masasi, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho Siku ya Posta yaliyofanyika leo Jijini Mwanza

No comments:

Post a Comment