KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 2, 2016

WENGI HAWAIFAHAMU NEC

kai1
Hussein Makame, NEC
Watanzania wengi hawaijui Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), majukumu yake na miongozo inayoongoza uchaguzi, hali inayosababisha manung’uniko mengi na upotoshaji kwa umma juu ya tume hiyo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani wakati akitoa tathmini ya elimu ya mpiga iliyotolewa hivi karibuni kwenye Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika wiki mbili zilizopita mjini Musoma.
Bw. Kailima alisema kutokana na hali hiyo, NEC imeanza kutekeleza mkakati kabambe wa kutoa elimu ya mpiga kura kupitia njia mbalimbali ikiwemo kushiriki kwenye maonesho na mikutano inayojumuisha wadau muhimu wa uchaguzi.
Alisema kutokana na utekelezaji huo wa mkakati wa elimu ya mpiga kura anaamini baada ya miaka mitano au kumi ijayo Watanzania wataifahamu tume hiyo na kufanikisha chaguzi zijazo bila ya manung’uniko na kwa mafanikio makubwa zaidi.
“Baada ya miaka 5 au 10 ijayo, tunategemea kwanza watu wataijua Tume ya  Taifa ya Uchaguzi kwa sababu bila kumung’unya maneno watu hawaijui Tume ndio maana wanauliza “hivi baada ya uchaguzi nyinyi tume mnafanya nini” alisema Bw. Kailima na kuongeza kuwa:
“Sasa wakiijuia Tume na ule uhalali wake, uiaminifu wa wananchi kwa NEC utaongezeka kwa kiwango kikubwa sana, manung’uniko kwamba tume haitimizi wajibu wake yatapungua kwa kiwango kikubwa ”
“Pili ule upotoshaji itapungua kwa sababu wananchi watakuwa wameelewa kwa kiwango fulani kuhusu Tume, taratibu za uchaguzi na wakishaelewa wewe ukienda na jambo lako watakushangaa.”

No comments:

Post a Comment