Mchezaji wa timu ya Yanga Thaban
Kamusoko akikokota mpira mbele ya Ibrahim Ajib mchezaji wa timu ya Simba
pia ya jijini Dar es salaam wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom
uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam timu hizo
zikitoshana nguvu kwa kufungana magoli 1-1 huku timu ya simba ikicheza
pungufu kwa muda mrefu baada ya mchezaji wake Jonas Mkude kutolewa kwa
kadi nyekundu na mwamuzi wa mchezo huo.
Goli la timu ya Yanga limefungwa
na mchezaji Hamisi Tambwe katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo huku
timu ya Simba ikisawazisha kwa mpira wa kona katika kipindi cha pili
kupitia kwa mchezaji wake Shiza Kichuya ambaye alipiga kona na kujaa
wavuni moja kwa moja huku akiacha mshangao kwa wachezaji wa Yanga ambao
walikuwa tayari wamekaa golini ili kuodoa mpira huo bila mafanikio.
Timu za Simba na Yanga zikiingia uwanjani kabla ya mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Wachezaji wa timu za Simba na Yanga wakisalimiana kabla ya mchezo huo.
Kikosi cha Simba kikiwa katika picha ya pamoja.
No comments:
Post a Comment