YANGA YASEMA NI UZUSHI BADO HATUJAINGIA MKATABA NA LWANDAMINA TOKA ZAMBIA,TUNA IMANI NA MWAMBUSI.
Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Timu ya Yanga imekanusha taarifa
zinazozagaa kwenye mitandao kuwa wameingia mkataba na kocha kutoka
Zambia kwa ajili ya kuchukua mikoba ya Hans Van Der Pluijm aliyetangaza
kujiuzulu kutokana na kukerwa na baadhi ya matamshi ya uongozi huo.
Akizungumza na FULLSHANGWEBLOG.COM,Kaimu
katiba Mkuu wa klabu hiyo Baraka Deusdedit,amesema kuwa mpaka sasa kuna
majina matano ya makocha ambao wameleta CV zao kwa ajili ya kuomba
kuifundisha Yanga hivyo mashabiki watulie kipindi hiki na kuacha
kusikiliza maneno ya watu kwani bado hatujaingia mkataba na George
Lwandamina.
“Tunaomba watu watuelewe kuwa sisi bado
hatujaingia mkataba wowote na kocha huyu ila hata yeye tayari kaleta CV
yake na kamati yaa utendaji itakaa na kupitia majina hayo na itatangaza
na pia watu wajue kuwa George Lwandamina bado ana mktaba na timu yake ya
Zesco United na unatarajia kumalizika mwakani,”alisema Deusdedit
Aidha amewataka mashabiki na wanachama wa
klabu hiyo kuwa wasiwe na wasiwasi muda sio mrefu kamati ya usajili
itakaa kwa pamoja na kupitia hayo majina hivyo wataweza kutangaza jina
la huyu kocha atakayepita kuchukua mikoba ya Hans Van Der Pluijm.
iIla kwa sasa timu ipo chini ya Kocha
Msaidizi Juma Mwambusi na kesho anatarajia kuiongoza itakapocheza kiporo
chake dhidi ya wanajeshi JKT Ruvu katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es
salaam.
Kwa upande wa Pluijm leo alitinga
mazoezini na kuwaaga wachezaji wake pamoja na benchi la ufundi na kutoa
wosia kidogo kwa wachezaji na kuwataka wapambane ili wawezi kutetea
ubingwa msimu huu na kuendelea kuwa na nidhamu ya hali ya juu kwa benchi
jipya litakalotangazwa.
No comments:
Post a Comment