KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 22, 2017

WAKINA MAMA NA WATOTO WAENDELEA KUPATA FARAJA WILAYANI SENGEREMA




o   Ni kupitia mradi wa kutokomeza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga
o   Na kurahisishwa na Huduma ya M-Pesa ya Vodacom
 Wakina mama wajawazito na watoto wa wilayani Sengerema wamefarijika baada ya kujionea manufaa ya mradi wa kutokomeza vifo vya akina mama hao na watoto wachanga ukiendelea vizuri na kuleta mabadiliko makubwa katika jamii yao inayowazunguka,Mradi huo ambao ulizinduliwa mwaka jana wilayani humo  chini ya ufadhili wa taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation kwa kushirikiana na  mashirika ya kimataifa ya USAID, Path Finder na Touch Foundation unazidi kuleta mafanikio makubwa katika wilya hiyo.
 Moja ya mafanikio makubwa ambayo yamepatikana kupitia mradi huu ni kuokoa maisha ya wanawake wajawazito na watoto wachanga wapatao 580 pia umewezesha mafunzo  kwa wahudumu wa Afya wa ngazi ya Jamii wanaopita kila kaya kutoa elimu, ili kubadili mitazamo hasi ya baadhi ya akina mama kutofika kwenye vituo vya afya kupatiwa huduma za uzazi na akina mama zaidi ya 6,000 wamepatiwa elimu hii.
Wafadhili wa mradi huu  wamekuwa wakigharamia mafunzo kwa wahudumu wa afya na usafiri wa akina mama wajawazito wanaokaribia kujifungua kuwawahisha kwenye vituo vya afya kupata matibabu ya haraka pindi panapohitajika msaada ambapo wameingia mkataba maalumu na madereva wa teksi katika kufanikisha mradi huu ambao hutoa huduma hii kwa haraka na kulipwa  kupitia huduma ya M-Pesa.
Mkazi wa Sengerema Mwanza Kwangu Jackson, ambaye ni mmoja wa wanawake walionufaika akiongea kwa niaba ya wanufaika wa mradi  aliupongeza mradi huu na kusema ni mkombozi kwa akina mama wengi  na ulimsaidia alipokuwa mjamzito na kwenye hali ya uchungu. Alipopiga simu aliweza kusaidiwa mara moja na amejifungua salama kabisa na anatoa wito kwa wanawake wengine wengi zaidi kujitokeza kunufaika na huduma hii.
 “Kipindi changu cha ujauzito kiligubikwa na changamoto mbalimbali ,ulipofikisha miezi 8 nilianza kusikia maumivu makali kwenye kiuno na nilitembea umbali wa kilometa 2 hadi kituo cha afya ambapo mhudumu aligundua kuwa nilitakiwa kujifungua kwa njia ya operesheni na kulazimika kunihamishia katika hospitali ya wilaya iliyopo umbali wa Kilometa 55 ambapo nilisafirishwa na teksi iliyopo chini ya mradi huu ambayo ilitumia muda wa  masaa 2 kufika hospitalini hapo ambapo niliweza kujifungua salama.Bila huduma hii ningepoteza maisha yangu na mtoto”.Alisema.
 Akiongea wakati wa uzinduzi wa mradi huu,Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dk.Hamis Kingwangalla,aliwapongeza wadau wote walioufanikisha na kuwa unaenda sambamba na malengo ya serikali  ya kutokomeza matukio ya vifo vya wanawake wajawazito na watoto wachanga nchini.
Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia,alisema mfuko wa kusaidia jamii wa kampuni hiyo pamoja na kampuni kwa ujumla inajivunia kuona mafanikio makubwa yanapatikana katika  kipindi kifupi  cha mradi huu wenye lengo la kuunga mkono jitihada za serikali za kuboresha sekta ya afya nchini na adhma ya kutokomeza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga nchini.
“Mradi huu ambao unajulikana kama”MOYO” awamu ya pili umelenga kuunga mkono jitihada za serikali za kuboresha sekta ya afya nchini na adhma ya kutokomeza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga nchini pia umelenga kurejesha fadhila kwa wateja wetu, tutagharamia usafiri wa akina mama wajawazito kupitia huduma ya M-Pesa kama ambavyo ilikuwa kwenye awamu ya kwanza ya mradi ili waweze kufika kwenye vituo vya afya kupata matibabu haraka“,Alisema.

No comments:

Post a Comment