KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

March 29, 2017

ORODHA YA MAJINA YALIYOPITISHWA NA KAMATI KUU CCM KUGOMBEA UBUNGE AFRIKA MASHARIKI

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza majina ya wanachama wake 12 walioteuliwa kugombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki, uchaguzi unaotarajiwa kufanyika kwenye mkutano wa Bunge ujao.

Akisoma majina hayo leo wakati wa Mkutano na waandishi wa habari, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amesema kuwa wameteua wananchama hao miongoni mwa wengi zaidi ya 400 waliokuwa wamechukua fomu kugombea nafasi hizo.

Mchanganuo
Miongoni mwa wabunge 9 watakaokwenda Bunge la Afrika Mashariki kuiwakilisha Tanzania, 6 watatoka CCM. Kufuatia idadi, hiyo CCM imesema kuwa itatoa wabunge watatu wa kiume na watatu wa kike ambapo miongoni mwao wanne watatokea Tanzania Bara na wawili watatokea Tanzania Visiwani.

Walioteuliwa kugombea nafasi hizo ni;

Wanawake Tanzania Bara;
  1.     Zainabu Rashid Mafaume Kawawa
  2.     Happiness Elias Lugiko
  3.     Fancy Haji Nkuhi
  4.     Happiness Ngoti Mgalula
Wanaume Tanzania Bara;
  1.     Dkt Ngwaru Jumanne Maghembe
  2.     Adam Omari Kimbisa
  3.     Anamringi Issay Macha
  4.     Charles Makongoro Nyerere
Wanawake Zanzibar;
  1.     Maryam Ussi Yahya
  2.     Rabia Abdallah Hamid
Wanaume Zanzibar;
  1.     Abdallah Hasnu Makame
  2.     Mohammed Yussuf Nuh
Miongoni wa wagombea hawa 12, Bunge litapiga kura kuchagua wabunge sita watakaoiwakilisha Tanzania kwenye Bunge la Afrika Mashariki kwa tiketi ya CCM.

No comments:

Post a Comment