KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

March 27, 2017

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA KUMWAKILISHA MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA SULUHU HASSAN TAMASHA LA PASAKA

MSA1
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akitangaza mgeni rasmi wa Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika Aprili 16 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Msama amemtaja Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mh. Mwigulu Nchemba kuwa ndiye atakuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan.
Ameongeza kuwa maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri na karibu mambo mengi yako tayari kwa ajili ya tamasha hilo litakalofanyika pia katika mikoa kadhaa, Ambayo ni Simiyu, Dodoma Iringa, Mwanza na Geita.
MSA2
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye mgahawa wa Break Point Kinondoni jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment