
Wajumbe wa Kikao cha Pamoja kati
ya Chama cha Ushirika cha Wauza Madagaa cha Tusiyumbishane kilichopo
eneo la Maruhubi mjini Unguja na ugeni wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo
Tanzania (TADB). Kikao kilijadilia changamoto zinazozikabili Ushirika
huo na namna TADB inavyoweza kuwasaidia katika kuendeleza ushirika huo.

Mtaalamu wa Ushirika kutoka Wizara
ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Bw. Khamis Mkanga
(katikati) akiendesha Kikao cha Pamoja kati ya Chama cha Ushirika cha
Wauza Madagaa cha Tusiyumbishane kilichopo eneo la Maruhubi mjini Unguja
na ugeni wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Kulia ni
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (kulia).



No comments:
Post a Comment