
Waziri wa Kilimo, Maliasili,
Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (kushoto)
akimkabaribisha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya
Kilimo ya Tanzania (TADB), Bw. Francis Assenga (kulia) wakati
walipomtembelea Ofisini kwake mjini Unguja.

Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara
wa TADB, Bw. Augustino Chacha (wapili kushoto) akikaribishwa na Waziri
wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid
Mohamed (kulia) wakati viongozi wa TADB walipomtembelea Mhe. Waziri
Ofisini kwake mjini Unguja. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji
wa TADB, Bw. Francis Assenga (wapili kulia) na Meneja Mikopo wa TADB,
Bw. Samuel Mshoto.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo
anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi Maryam Juma Abdullah
(aliyesimama) akizungumza wakati ugeni kutoka TADB ulipomtembelea Waziri
wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid
Mohamed Ofisini kwake mjini Unguja.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB,
Bw. Francis Assenga (aliyesimama) akieleza dhima ya Benki ya Kilimo
wakati walipomtembelea Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi
Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (wapili kulia).


No comments:
Post a Comment