Kozi ya waamuzi wa mpira wa miguu,
iliyolenga kuwainua madaraja kutoka madaraja waliyonayo sasa hadi
ngazi moja juu, imesogezwa mbele kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya
Waamuzi ya TFF, Saloum Chama.
Chama amesema kwamba kozi hiyo
iliyopangwa kufanyika kuanzia Juni 29, mwaka huu itafanyika hapo baadaye
katika tarehe itakayopangwa, lakini itakuwa ni kabla ya Uchaguzi Mkuu
wa TFF.
“Watu wasiende kuripoti hiyo Juni
29, mwaka huu kama tulivyotangaza. Tumesogeza mbele kidogo kozi hii.
Tarehe mpya itatangazwa hapo baadaye,” amesema Chama ambaye alitaja
vituo vilivyopangwa kuwa ni Mwanza, Ruvuma na Dodoma
No comments:
Post a Comment