Marekani inapanga kupiga marufuku
raia wake wasisafiri kwenda Korea Kaskazini, kwa mujibu wa mashirika
mawili ya kupanga safari ambayo yanafanya kazi humo.
Mashirika
hayo ya Koryo Tours na Young Pioneer Tours yamesema marufuku hiyo
itatangazwa tarehe 27 Julai na itaanza kutekelezwa siku 30 baadaye.Seriakli ya Marekani bado haijathibitisha taarifa hizo.
Young Pioneer Tours ndio waliofanikisha mwanafunzi Mmarekani Otto Warmbier kuzuru Korea Kaskazini.
No comments:
Post a Comment