Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Bw.
James Ihunyo (wapili kushoto) akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa
miradi iliyokopeshwa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB)
wilayani humo. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw.
Francis Assenga (katikati) na viongozi waandamizi kutoka wilayani na
Benki ya Kilimo.
Makamu Mwenyekiti wa Skimu ya
Umwagiliaji ya Mkula, Bw. Mohamed Dadi (kushoto) akionesha maendeleo ya
Skimu hiyo wakati Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Bw. James Ihunyo (wapili
kulia) pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga
(katikati) na viongozi waandamizi kutoka wilayani na Benki ya Kilimo
walipotembelea Skimu hiyo.
Kaimu Afisa Tarafa ya Mang’ula,
Bw. Omary Said (kulia) akitoa maelezo kuhusu Mradi wa Kilimo Shadidi
kinachofanyika katika Kijiji cha Msolwa Ujamaa kwa Mkuu wa Wilaya ya
Kilombero Bw. James Ihunyo (kushoto) na Umoja wa Wakulima wa Miwa wa
Msolwa Ujamaa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga
(katikati). Wengine wanaosikiliza na viongozi waandamizi kutoka wilayani
na Benki ya Kilimo.
No comments:
Post a Comment