KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 21, 2017

SERIKALI ZA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI ZASAINI MKATABA WA MAKUBALIANO YA KUTEKELEZA PROGRAMU YA URITHI WA UKOMBOZI WA BARA LA AFRIKA


01
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Tanzania Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akisaini Mkataba wa Makubaliano kati ya Tanzania na Afrika Kusini wa namna ya kutekeleza Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika kwa lengo la kukusanya, kuhifadhi, kuendeleza na kuzitunza urithi huo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo mjini Dodoma jana Tarehe 19 Septemba 2017. Kushoto ni Waziri wa Sanaa na Utamaduni, Afrika Kusini Mhe. Nathi Mthethwa.

03

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Tanzania Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akibadilishana Mkataba wa makubaliano wa kutekeleza Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika na  Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa Afrika Kusini Mhe. Nathi Mthethwa mara baada ya kusaini mkataba huo mjini Dodoma jana Tarehe 19 Septemba 2017.

04

Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Tanzania Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na viongozi kutoka Tanzania na Afrika Kusini waliohudhuria hafla ya utiaji saini Mkataba wa Makubaliano wa kutekeleza Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika mjini Dodoma jana Tarehe 19 Septemba 2017.

No comments:

Post a Comment