Imamu
wa Msikiti wa Al Masjid Kirumbi Islamic Center uliopo Kimara amewazuia
waumini wake kutoshiriki katika kuvunja au kutoa kitu chochote katika
msikiti huo ambao unatakiwa kuvunjwa na Wakala wa Barabara Tanzania
TANROADS.
Imamu
wa Msikiti huo Ramadhan Juma amesema hayo jana wakati akifanyiwa
mahojiano na MCL na kudai kutokana na imani yao ni kosa kubwa mtu yoyote
kuvunja nyumba ya ibada kwa kuwa hiyo ni nyumba ya Mungu na kusema wao
hawajatoa kitu chochote zaidi ya vitu vidogo ambavyo vinatumika kusaidia
jamii kama jeneza.
"TANROADS
wametupa barua ya kuvunja msikiti ndani ya wiki moja kwa kile
wanachodai umevamia eneo la barabara hivyo walitaka tutoe vifaa ndani ya
wiki moja kupisha zoezi la barabara lakini kutokana na imani yetu na
Uislam unavyotufundisha ni kosa kubwa kuvunja nyumba ya 'Allah Subhanahu
Wa Ta'ala'
"Hii
ni nyumba ya ibada hivyo hatutainua mikono yetu kwa kujihukumu sisi
wenyewe kwa amri ya dini yetu ya Kiislam kwetu sisi ni kosa mtu kutoa
mkono wake kutoa sijui bati au chochote kile kinachohusu msikiti kwa
hiyo ndiyo maana tumeshindwa kuvunja msikiti huu" alisisitiza Imamu
Ramadhan
Hata
hivyo Imamu alisisitiza kuwa wao wameiachia serikali na hao TANROADS
waweze kubomoa wenyewe na kusema yeye amewakataza waumini wake
wasishiriki cha chochote katika kubomoa nyumba hiyo ya ibada
"Nimewaambia
waumini wangu wasitoe chochote katika kuvunja kwa msikiti huu, tutatoa
vitu vidogo vidogo ambavyo vinasaidia jamii kama vile jeneza na
vinginevyo tumevitoa lakini katika majengo kwa chochote kile tunawaachia
wenyewe, hii ni nyumba ya Allah hivyo wavunje wao halafu Mungu mwenyewe
ndiye atajua kwa kuwa hiyo ni nyumba yake atakavyohukumu yeye ndiye
anajua kwa kuwa hiyo ni nyumba yake" alisema Imamu Ramadhan Juma
No comments:
Post a Comment